Polepole yamemkuta vipi kwa Falahi?
ADELADIUS MAKWEGA-MBEYA
Disemba 17, 2021 Kamati ya Maudhui
ya TCRA imetoa hukumu dhidi ya Runinga ya Mtandaoni ya Mbunge wa Bunge la Jamuhuri
ya Muungano wa Tanzania Ndugu Humphrey Polepole kwa kituo hicho kupewa onyo
kali, pili kipindi cha Shule ya Uongozi kusisimashwa kwa muda hadi awe na
wafanyakazi wa taaluma ya uhandishi wa habari na utangazaji ili kuleta ufanisi
na tija katika kazi yake na vipindi vyake visingatie misingi ya uhandishi wa
habari.
Kama nionavyo mimi maamuzi
haya ya kamati hii hayakuwa na haki bali ni uonevu kwa kuwa wajumbe wawili Haji
Gunze na Jacob Tesha hawakutumia ipasavyo taaluma zao na uzoefu wao kuliamua
jambo hilo.
Kulingana na taaluma ya
habari na utangazaji, kuna aina mbambali ya vipindi katika Redio/Runinga kwanza
kuna vipindi vya mahojiano haya yanakuwa katika mtindo wa maswali na majibu huku
muda wake unategemea mahitaji ya chombo. Pili kuna vipindi vya makala hapa
inategemea na maamuzi ya mtayarishaji na kuna wakati mwingine hata maswali na
majibu inaweza kuwa makala huku ikiwa na vyanzo vya kutosha, muda wa makala
unategema chombo husika.
TBC 1/TBC Taifa makala zao
ni kati ya dakika 5-29.Tatu kuna ripoti za kawaida kama zile za matukio
mbambali kwa kina inaweza kuwa ya kati ya dakika 2-4, lakini pia kuna habari za
taarifa ya habari ambazo hizo Jacob Tesha mjumbe mmojawapo wa kamati hii ndizo
alikuwa anazisoma tangu External service/RTD/DW KISWAHILI hapa msikilizaji atasiki Lindi–Watu 100 hawana…Nairobi-Rais
Uhuru Kenyatta wa Kenya amekutana…, Dar
es Salaam-Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ndugu Godwin Gondwe ametoa wiki…
Kuna kitu kingine ambapo
huwa kuna vipindi vinavyofanywa na wenye taaluma /ujuzi huo. Hapa ndipo
unapokutana na vipindi vya shule ambavyo vinakuwa kwanza vya muda mrefu kati ya
dakika 40-120. Kwa kuwa kunakuwa na muhtasari(silabasi) ilikuukamilisha huo
muhtasari kunakuwa na vipindi 1-40 kulinga na mahitaji ya muhtasari huo.
Episode moja muda wake unategemea sana hiyo redio /Runinga inarusha matangazo
yake kwa muda gani. Mathalani TBC episode moja inaweza kuwa kati ya dakika 14(15),
28 (30) au dakika 54 (60) kwa kuwa TBC wanatangaza saa 24.(Muda nilioweka
katika mabano unahusisha na dakika za viashiria /signature tune vya katika kila
episode moja.
Hapo nikumbushe jambo moja
enzi za RTD kulikuwa na vipindi vya shule ambapo mwalimu alikuwa akifundisha na
baadhi ya shule walikuwa wakifuatilia hilo. Palikuwa inasikika mandhari ya
darasa huku wanafunzi wa studio wakiulizwa maswali na kujibu naye mwanafunzi
anayesikiliza akiulizwa maswali na badaye majibu sahihi kutolewa kwa somo hilo.
Hapa masomo kama Historia, Jiografia, Kiswahili,Kiingereza nakadhalika
yalifundishwa. Nakumbuka hata baadhi ya shule walikuwa na ratiba ya vipindi vya
redio kwa masomo yaliyokosa walimu na ratiba hizo zilikuwa zikitolewa na RTD tu
mara baada ya shule kufunguliwa.
“Utasikio leo ni Jiografia
darasa la tano, wanafunzi…”
Hata katika redio za kimataifa
mathalani NHK, BBC, na DW wanavyo vipindi vya Jifunze lugha na michezo maalumu
ya maigizo yenye lengo maalumu. Haya ni madarasa yenye kutoa elimu kama shule
yakiwa na vipindi 1-30 (Episode) kulingana na mahitaji yao nakulingana nafasi
wanavyokuwa hewana. Vipindi hivi vina nia ya kueneza utamaduni wao wa kutumia
lugha, kufundisha juu ya magonjwa mbalimbali na hata siasa.
Mfano mzuri kabisa ambao
naukumbuka ni madarasa yale ya RADIO D yalikuwa mafunzo ya Kijerumani ya hatua
A1 na A2. Hatua A1 ilikuwa na kipindi cha 1 hadi 26 na hatua ya A2 ilikuwa na kipindi
cha 27-52.
Hili kuitendea haki matini haya
naomba nikumbushe tu hatua A1 kipindi cha 24, kipindi hicho kilipewa jina
Dawati la Mhariri, kilizungumzia habari juu ya waandishi Paula na Philipo
walivyoripoti nadhani habrai ya nyangumi aliyeonekana jirani na ufukwe na
mizengwe kadhaa iliyotokea.
“Unasikiliza Radio D mafunzo
ya Lugha ya redio ambayo ni mafunzo ya ubia baina ya taasisi ya Goethe na Deutsche
Well ambayo yameandikwa na Bibi Merald Meeze…” Ndivyo yalivyonza mafunzo hayo
ya lughwa yaliyowahi kurushwa hewani na DW Kiswahili.
Katika vipindi kama hivyo mfundishaji
anaweza kuzungumza mwanzo hadi mwisho, anaweza akatumia michoro, picha kama
anatumia runinga, pia anaweza akatumia vichekesho, michezo ya kuigiza, mashairi
na nyimbo ilimradi ujumbe kufika kwa mwanafunzi wake.(hadhira)
Ndiyo kusema hii Shule ya Uongozi
ilikuwa kama madarasa ya Radio D ya Bibi Merald Meeze, pia kama vile vipindi
vya shuleni vya RTD na TBC na STARTV na ITV wakati wa wimbi la kwanza la Korona
ambapo shule zilifungwa, runinga na redio zilikuwa sehemu ya madarasa kwa
masomo mbalimbali.
Ndugu Polepole amekuwa Katibu
wa Uenezi wa CCM na sasa ni mbunge na amefanya kazi kwa karibu sana na Marehemu
John Magufuli anatambua mambo yanavyofanyika katika siasa za Tanzania kwa kina,
kwa hiyo akaamua kutoa elimu kwa nduguze Watanzania.
Vipindi hivi vimekuwa vya
saa karibia mbili na mwisho alitoa nafasi ya maswali ambapo alipata mrejesho
iwe kwa ujumbe, kupigiwa simu au watu kutoa maoni katika kurasa zake za
mitandaoni ikiwa sawa sawa na vipindi vile vya Radio D vya DW vya Bi Merald
Meeze ambapo msikilizaji aliyekuwa anajifunza Kijerumani aliweza kuandika barua
ya maswali kwa mtayarishaji na akajibiwa.
Kumbuka jambo moja la msingi
msomaji wa matini haya kuwa huyu Ndugu Polepole yeye anafundisha darasani na ndiyo
maana alikuwa na ubao wake kupitia runinga. Yeye hapa hafanyi ripoti kwa ajlii
ya taarifa za habari, hafanyi ripoti kwa ajili kipindi cha majira, hafanyi
kipindi cha maswali na majibu na wala hafanyi makala kama zile za TBC ambazo
nilizielezea kwa kina kule juu. Yeye anafundisha kama darasani katika shule yake
ambayo muhtasari wake au mwongozo anao yeye mwenyewe kama yalivyokuwa mafunzo
ya jando na unyago.
Kwa sasa watu wengi
wamesoma, shuleni mwalimu anatayarisha somo lake alafu anaenda kulifundisha fu
darasani, kisha anatoa nafasi ya maswali mwishoni akimaliza atafunga kipindi
mtakutana naye kipindi kijacho kwa mujibu wa silabasi yake.
Kwa hoja ya maadili ya uandishi
wa habari katika shule ya uongozi nadhani siyo pahala pake kabisa kama ilivyo
kwa watayarishaji wa vipindi vya RTD vya shule na kipindi cha Radio D cha Bi
Merald Meeze labda yale maadili ya ualimu na sina hakika kama kama Ndugu
Polepole alinukuliwa akitoa tusi.
Kwa hoja ya misngi ya
uhandishi wa habari ya mizania hapa haisuki kabisa. Kwa mfano mwalimu wa
Historia darasa la sita anayefundisha namna wamisionari walivyoshiriki katika
ukoloni alafu unamwambia aletwe pardiri aje kusema upande wake, hapo
haikubaliki kabisa ni kuliharibu darasa hilo. Hapo linalo fundishwa ni
kulingana na muhtasari wake wa somo hilo.
Kwa hoja juu ya kuajili
watangazaji wenye sifa za utangazaji na uandishi wa habari si sahihi hii ni
shuleni. Runinga, redio, youtube na mitandao ya kijamii inapitia tu na ndiyo maana
Ndugu Polepole anaweza hata akafundisha katika chumba au ukumbi na shule
ikaendelea kama alivyokuwa akifanya baadhi ya maeneo aliyoalikwa.
Hapo ninavyoona kwa maamuzi
wa TCRA ni kama wanamwambia kuwa Ndugu Polepole aende akajifunze taaluma ya uandishi
wa habari au awe aje mtu aliyesoma taaluma hiyo alafu amualika yeye kama mgeni
ambalo nadhani hilo ni jambo halikubaliki.
Kuhusu watumishi wake kuwa
na taaluma ya habari na utangazaji waliokuwa wanatumika ni wajuzi wa sauti,
michoro na picha za mnato na video tu. Yeye hana shida ya mhariri. Kama
walivyofanya RTD na TBC kwa mafundi mitambo ambao wanafanya vipindi vya shule
kwa kurekodi.
Niliwahi kuambiwa na rafiki
yangu mmoja ambaye wakati huo akiwa mwanafunzi wa sheria Hendry Msaki ambaye
sasa amefariki kuwa panapofanyika maamuzi yoyote juu ya jambo lolote lile hulka
ya yule anayeamua jambo hilo huwa ni
kitu cha msingi sana hata katika muktadha wa kimahakama.
Aliniambia kuwa mathalani
katika kesi za mauwaji kuna majaji huwa wana hulka mara zote katika kuhukumu kesi
hizo za mauwaji wapo wanaotoa hukumu ya kifungo cha maisha badala ya ile ya
kunyongwa hadi kufa. Wengine akigundua kuwa mshitakiwa kulingana na ushahidi
ameua kwa kukusudia lazima hukumu ya kunyongwa hadi kufa itatolewa. Bila ya
kujali kuwa hapa jaji sheria inampa nafasi ya kuchagua upande fulani.
Binafsi naona kamati chini
ya Mwenyekiti Haji Gunze na wajumbe wake Jacob Tesha na Dereck Mujuruni hawakutumia
vizuri nafasi zao na taaluma zao katika kuliamua jambo hilo. Kitendo cha
kuitumia sheria kila mara katika taaluma ya habari kinadumaza kazi hii, kwa
kuwa sheria ni sehemu ndogo sana ya uwanahabari.
Katika wajumbe wa kamati hii
ambaye kidogo anaonekana anafahamu suala la utangazaji ni Jacob Tesha. Yeye
kulingana na wasifu wake ana Shahada ya Kwanza Uongozi na Mahusino ya Kimataifa
na Shahada ya Pili ya Mawasiliano ya Umma. Ambapo kwa utafiti wangu nilibaini
kuwa elimu hiyo aliipata akiwa tayari mtumishi wa RTD.
Nimebaini kuwa kwa sehemu
kubwa utangazaji alijifunzia akiwa kazini RTD huku sauti yake iliwavutiwa RTD
kumuajili kama mtangazaji wakati huo. Pia amewahi kufanya kazi ya Shirika la
Utangazaji la Ujerumani (DW Kiswahili). Nionavyo mimi kwa sehemu kubwa Jacob
Tesha alitakiwa kuwaongoza wenzake katika kusaidia kuutatua mgogoro huo ambao
ulikuwa ni mdogo tu.
Kwa mfano kwa heshima yake
Ndugu Polepole angeshauriwa kipindi chake kisiwe darasa sasa kiwe kama Makala,
hapo mngemtafutia vijana wazuri kutoka TBC, Azam TV, ITV au STAR TV
wakamuongoza kwa muda wa mwezi mmoja mkatazama muelekeo wake hakika angekuja na
makala nzuri sana. Au Tanzania kwa sasa mtu akitoka katika nafasi yake hapaswi
kuheshimika?
Katiba yetu ya Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania 18 (2) kuna wakati iliesema kuwa
“Kila raia anayo haki ya
kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote
ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala
muhimu kwa jamii.”
Kukimbilia kufungia vyombo
haina tija kwa kuwa wenye vyombo binafsi wanaisadia mno serikali ila wanapaswa
kulelewa vizuri kwa kuaminiana, Kwa mfano kama Ndugu Polepole ambaye ni Mbunge
wa kuteuliwa na Rais na amewahi kuwa katibu uenezi wa CCM taifa, TV yake
inafungiwa kwa hoja hizo inakuwaje kwa mtu wa kawaida anaweza kuwekeza katika
biashara ya vyombo vya habari? Sote ni Watanzania tujitahidi kulitazama hili
kwa kina.
Wizara husika na TCRA
wajitahidi sana kuwa na aina ya wajumbe wa Bodi/kamati wenye mchanganyiko mzuri
siyo tu wale waliowahi kufanya kazi na serikali na kuwa jirani na viongozi
wakubwa mathalani haji Gunze amefanya kazi na Waziri Mkuu enzi za Jaji Warioba
kama msaidizi wa Habari na Jacob Tesha kafanya kazi na Mizengo Pinda.. Wakiwa
na mlengo wa utii wa kila jambo. RTD /TBC na sasa ITVna magazeti mengi ya
zamnai wanao watumishi wengi waliostaafu na wana uzoefu mkubwa watumiwe katika
Bodi/kamati za utangazaji wapo majumbani wakicheza na wajukuu watumike na siyo
majina yaleyale. Kwa leo naweka kalamu yangu chini hapo, nikukutakia siku
njema.
0717649257
No comments
Post a Comment