Zinazobamba

WATANZANIA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA KATIKA SOKO KUU LA AFRIKA.

Wanawake na vijana wametakiwa kuamka na kuchangamkia fursa zipatikanazo katika soko Huru la Afrika kwa kuwa wabunifu na kufanya utafiti wa bidhaa zinazohitajika kwa wingi katika soko hilo.

Muwakilishi wa nchi katika Bunge la vijana la dunia Mansouza Kingu akiongea na wanasemina za jinsia na maendeleo(GDSS) jijini Dar es salaam.

Hayo yameelezwa mapema wiki hii na Muwakilishi wa nchi katika Bunge la vijana la dunia Mansouza Kingu katika mfurulizo wa semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS) zinazofanyika kila jumatano makao makuu ya TGNP Mabibo jijini Dar es salaam.

Aidha Mansouza amewaambia kuwa fursa moja wapo ya soko hili ni kuondolewa kwa vizuizi mbalimbali vya kibiashara baina ya taifa moja na jingine barani afrika.

Na pia kwa hapo baadae itakuwa na kuvuka mipaka bila passport kwa mataifa ya ndani ya bara la Afrika kama Agenda ya Umoja wa Afrika ya mwaka 2063 ya afrika tuitakayo inayotaka Afrika iwe moja na vizuizi vyote viondolewe.

Ameendelea kusema kwamba mpaka sasa nchi zilizokubali kusaini makubaliano hayo ni nchi 54 za barani Afrika na nchi 41 mpaka sasa zimeshaanza kulasimisha hili zoezi Tanzania ikiwemo.

 “Na hii inatupa picha ya kwamba muamko umekuwa ni mkubwa sana hivyo sisi kama Watanzania tunatakiwa kuchangamka ili tusiwatengenezee mazingira wenzetu waje kunufaika kupitia sisi” amesema Mansouza   

“Soko kuu la afrika linaenda kuwa soko kubwa Zaidi duniani toka kuanzishwa shirika la biashara duniani yaani (WTO) Word Trade Organization, lakini pia soko hili litakuza biashara ya afrika kwa asilimia 50 na hii ni faida kubwa kwa bara lote la afrika”. Amesisitiza Mansouza

Ameongeza kuwa kwa uwepo wa soko hili endapo litakamilika kwa kila kitu katika utekelezaji wake inakadiliwa kuwa DDP ya afrika itapanda kwa Billion 3.5 za kimarekani na kusaidia kukua kwa uchumi wa dunia kwa kiwango cha dola 75 milioni za kimarekani.

Na mwisho ameongeza kuwa elimu Zaidi inabidi itolewe kwa jamii, serikali na mashirika binafsi waweze kuwaelimisha wananchi namna ya kunufaika na soko hili kwani bila elimu watu wengi hawatajua kama kuna kitu cha aina hii na matokeo yake yatanufaika makundi machache yenye taarifa sahihi.

Mwanaharakati Msafiri Shabani akitoa ufafanuzi wa jambo katika semina za Jinsia na Maendeleo(GDSS).
Washiriki wakifuatilia mafunzo kwa umakini.
Muimbaji mashahiri maarufu Mzee Abdalaah Imba akitoa ufafanuzi wa jambo mapema wiki hii katika semina za GDSS.
Baadhi ya Washiriki wa semina wakifuatilia wanachofundishwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa TABWA Bi, Noreen Mawala akitoa neno mbele ya washiriki wa semina za jinsia na maendeleo.
Semina ikiendelea.

Hakuna maoni