Zinazobamba

WABUNGE WA UPINZANI WAGOMEWA KUFANYA MIKUTANO,SOMA HAPO KUJUA

Mkutano wa  Mbunge wa Jimbo la  Temeke(CUF) Abdallah Mtolea, uliopangwa kufanyika leo umezuiwa na Jeshi la Polisi kutokana na sababu zisizofahamika.

 Mtolea akizungmza na Mwandishi wa Muungwana  kwa njia ya ujumbe mfupi na kuthibisha kuwa Mkutano huo  aliolenga kuzungumza na  wananchi wa jimbo lake leo umezuiliwa  leo na kueleza kuwa  kikao hicho kilichopangwa kufanyika leo kimezuiwa.
Mtolea alithibitisha kikao hicho kitafanyika na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, atahudhuria.

hata hivyo jana  mkutano uliondaliwa na Katibu wa CUF wilaya ya Kinondoni, Juma Nkumbi, ulivamiwa na watu wenye silaha waliovalia   maski  na waandishi kadhaa walijeruhiwa katika tukio hilo.