WASOMI WAANZA KUTOMWELEWA RAIS MAGUFULI,WAZISHANGAA KAULI ZAKE,SOMA HAPO KUJUA

Dk. Azaveli Lwaitama ambaye ni msomi pamoja na
mchambuzi wa masuala ya siasa nchini, ameeleza kushangazwa na kauli ya
Rais John Magufuli kutaka kuifanya Ikulu ya Jijini Dar es Salaam kuwa jumba la
makumbusho, anaandika Pendo Omary.
Wiki liyopita Rais Magufuli
alitangaza azima ya kuingeuza Ikulu ya Magogoni kuwa, jumba la makumbusho ikiwa
ni hatua ya serikali kuhamishia ofisi zake kuu mjini Dodoma kabla ya mwaka
2020.
Akizungumza na Chanzo Changu Dk. Lwaitama
amesema “wazo la kuhamisha shughuli za Ikulu ni nzuri.
“…ila kuigeuza Ikulu kuwa makumbusho, haya sio
maamuzi mazuri. Hata kama Makao Makuu ya Ikulu yatakuwa Dodoma, ikumbukwe kila
mkoa kuna Ikulu ya rais hivyo ni busara makazi hayo yakabaki kama ofisi
za serikali kwa baadhi ya vitengo.
“… mfano, usalama wa taifa na baadhi ya watendaji wa
Ikulu. Kwa sababu ukweli ni kwamba, sio wafanyakazi wote wataenda Dodoma,”
amesema Dk. Lwaitama.