MZEE AKILIMALI AWAPIGIA "MAGOTI" WANA-YANGA, WENYEWE WASHINIKIZA AVULIWE UANACHAMA
Kufuatia taarifa ya kutuhumiwa na wanayanga juu ya kumtusi Mwenyekiti wa Klabu Yanga, Bw Yusuph Manji kuwa amekurupuka kuhusu kuomba ridhaa ya kukodishiwa klabu hiyo, Leo Mzee Akilimali ameibuka na Kuwaomba radhi mashabiki na familia nzima ya wana-yanga akisema haikuwa dhamira yake kumtukana na kwamba ni jambo ambalo linamnyima usingizi toka alipolitamka.
Mzee Akilimali amesema anaomba msamaha kwa kitendo hicho, na anaamini kuwa wanayanga watamuelewa kwani si nia ya mwanayanga yeyote kuharibu umoja na mshikamano uliopo.
"Kwa kweli Sijamtusi
mwenyekiti wangu kwa kusema amekurupuka. Neno hilo ni la kawaida wala
sikuwa na dhamira ya kumtusi mwenyekiti wangu, nawaomba radhi wana-Yanga
kwa kauli zangu. Usiku sijalala nilikosa raha mara baada ya kusikia
Manji kajiuzulu" Alisema Mzee akilimali.
Mie naomba tuwe na umoja tatizo letu na mwenyekiti ni kushindwa kutuita wazee kwenye mpango wake wa kuichukua timu.
Sisi
tunampenda na kumuhitaji sana Yusuf lakini tunahitaji aendeleze mfumo
wa zamani alioanza nao wa kujali na kuthamini wazee ili nasi tujisikie
vizuri na klabu yetu.
Nasisitiza
sina chuki na Manji maana kwa mdomo wangu huu nimeshiriki sana kumuweka
madarakani mpaka pale umma wa watanzania wakasema tumevunja katiba.
Ninachotaka alitambue Baraza la Wazee na sisi tukae nae tuzungumze
mstakabali wa klabu yetu.
Katika hatua nyingine Viongozi
wa matawi wa klabu ya Yanga leo saa nne walikutana katika kikao cha dharura
kufuatia mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji kutangaza kujiuzulu na
kutupilia mbali mpango wake wa kutaka kuikodisha timu hiyo na kuiendesha
kibiashara kwa miaka 10.
Taarifa za Manj kujiuzulu zilikuja kufuatia tuhuma kuwa kuna baaadhi ya viongozi wa Yanga
wamemkashifu na mmoja aliyetuhumiwa kwa kosa hilo ni Katibu Mkuu wa
Baraza la Wazee, Yahya Akilimali.
Katika kikao cha leo, Viongozi hao wa Matawi wamefikia maazimio haya, lengo likiwa ni kuleta mshikamano na umoja klabuni hapo.
- Viongozi wa Matawi wamemtaka Katibu Mkuu wa Yanga kumfuta uanachama wa Yanga Yahya Akilimali kwa kosa la kumkashifu mwenyekiti wa Yanga.
- Viongozi hao wamelaani taarifa iliyotolewa katika vyombo vya habari na Katibu wa Baraza la Wazee, Mzee Akilimali na kuwa haikuwa taarifa iliyopewa baraka na Yanga.
- Katiba ya Yanga hailitambui Baraza la Wazee badala yake inalitambua Baraza la Wadhamini, hivyo basi viongozi wa Yanga wamemuomba Katibu Mkuu wa Yanga kuvunja Baraza la Wazee na wazee hao warudishwe katika matawi wawe wanachama wa kawaida.
- Mwanachama yeyote wa Yanga atakayeongea na vyombo vya habari bila idhini ya Yanga, atakuwa amejifuta uanachama wake.