Zinazobamba

SOKO LA HISA LAWATANGAZIA NEEMA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU,SOMA HAPO KUJUA




 
 Pichani ni  Meneja Masoko wa DSE Patrick Mususa wakati wa mkutano na waandishi wa Habari

NA KAROLI VINSENT
SOKO la hisa mkoani Dar es salaam  (DSE) limewataka wanafunzi wa vyuo  vikuu nchini  kujitokeza kwa wingi katika  shindano la (Schollar investment challenge) ili kuweza kupata fursa mbalimbali za  kibiashara nakukuza uelewa juu ya utendaji kazi wa soko hilo kiuchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema hii leo jijini Dar es salaam Meneja Mauzo na Biashara wa DSE Partick Mususa amesema katika kuhakikisha  shindano hilo linafanikiwa taasisi hiyo imeamua kuwateua mabalozi  mbalimbali katika vyuo vishiriki katika shindano hilo ikiwa ni sehemu yakukuza hamasa juu yashindano hilo
 .
Mususa amesema Mabalozi watakaoteuliwa katika shindano  hilo  ni mabalozi kutoka vyuo mbalimbali vikuu ambavyo ni pamoja  na chuo kikuu cha Dar es salaam UDSM,Chuo Kikuu cha SOKOINE, Chuo cha usimamizi wa fedha IFM, Chuo kikuu cha Dodoma UDOM ,Pamoja na chuo cha Mipango miji Dodoma IRDP ,

Mususa ameeleza kuwa kupitia mabalozi wa vyuo hivyo wanategemea kupata   hamasa ya kushiriki kwa wanafunzi katika shindano hilo .

Mususa ameongeza kuwa kupitia mabalozi watakao teuliwa nasoko hilo la hisa la Dares salaam chuo ambacho kitakuwa na mabalozi wengi zaidi ndicho kitapewa nafasi zaidi yakushinda nakuweza kupewa fursa mbalimbali zinazo tolewa na soko hilo 
.
Mususa amebainisha kuwa  sambamba nakutoa hamasa kwa wanafunzi hao na kuweza kujiunga na shindano hilo aliviambia vyombo vya habari  kuwa  mabalozi watakao chaguliwa  na taasisi hiyo wataweza kupata fursa za kuwekeza katika makapuni mbalimbali yanayo uza hisa zake kupitia soko hilo.

"wanafunzi hawa wa vyuo vishiriki wa shindano letu la scholar invest ment Challenge  watatapatafursa mbalimbali ikiwemo kununua hisa na kudhaminiwa  na hata kupewa ajira baada ya kushiriki katika shindano letu "Aliendelea kueleza Meneja huyo wa Mauzo na Biashara
      

No comments