Zinazobamba

TUKIO KUBWA JIJINI DAR LEO,LHRC YAAZIMISHA SIKU YA HAKI ZA BINADAMU,JAJI MJULIA ATOA NENO,SOMA HAPO KUJUA

Bendi ya Jeshi la Polisi nchini nalo alikuwa nyuma kwenye maandamano ya kuazimisha siku ya Haki za Binadamanu nchiniyaliyofanyika kwenye Viwanja vya makumbusho jijini dar es Salaam,
Wanafunzi Mbali mbali nchini Wakiwe kwenye Maandamano ya kuazimisha siku ya Haki za Binadamu nchini,
Tukio hili ambalo limeaandaliwa na kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini,(LHRC)


Wito umetolewa kwa watanzania pamoja na Serikali kuruhusu lugha za asili kutumika kujieleza na kujitetea katika sehemu mbalimbali ikiwemo mahakamani.Anaandika KAROLI  VINSENT endelea nayo
        Akizungmza katika maadhimisho ya siku ya haki za binadamu iliyoandaliwa na kituo cha sheria LHRC iliyofanyika katika uwanja wa makumbusho ya Taifa leo Jijini Dar es Salaam, jaji wa mahakama kuu,Aloyce Mjulia amesema kuwa watu wengi wanahukumiwa kwa kushindwa kujieleza.

      Amesema endapo mtu atapewa frusa ya kutumia lugha anayiifahamu kwa kina ataweza kujieleza na kupata haki ya msingi.
       “Mimi nina uzoefu kwa kazi hizi mara nyingi hata askari wetu hawafuati masharti ya haki za binadamu kwani wanapowakata watuhumiwa wanahoji maswali ambayo wanajua kwamba watajibiwa wanavyopenda wao.,

“vile vile mahakamani mtu anatakiwa kujitetea kwa kutumia lugha ambayo anaijua kwa kina na awepo mtu wa kutafsiri lakini mara nyingi utakuta hii inatokea pale tu anapokuwepo raia wa bkigeni,”amesema Jaji Mjulia.
Mgeni Rasmi wa siku ya Haki za Binadamu nchini Jaji wa Mahakama kuu nchini Aloyce Mjulia akimkabidhi cheti cha Pongezi Mwangalizi wa uchaguzi kwa kazi nzuri aliyofanya 

Kwa upande wake Mwanasheria kutoka LHRC Bwana Sungusia amesema vitendo vya uvunjifu wa Haki za binadamu nchini vimeongezeka sana huku akitolea mfano kipindi kilichomalizika cha uchaguzi mkuu kwa kusema vyombo vya dola hususani polisi wamekuwa ni watu wakutekeleza vitendo vya kinyama kwa raia.
Picha ya pamoja kati ya Viongozi wa LHRC na waangalizi wa TACCEO



“Vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu vimeongezeka sana hapa nchini tumeshuhudia hata kipindi cha uchaguzi,maana hata sisi haki za binadamu tumekuwa waathirika wa kubwa,vifaa vyetu vy uangalizi mpaka leo vipo polisi,”amesem Sungusia.









Hakuna maoni