Zinazobamba

WAFANYABIASHARA WAMPUUZA MAGUFULI,NI AGIZO LAKE LA SIKU SABA,KOVA ATANGAZA ZAWADI NONO ATAKAYEMDAKA HUYU,SOMA HAPO KUJUA

Kamanda wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Suleiman Kova akionyesha picha ya Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya REGIONAL CARGO SERVICES LTD,ABDULKADIR S/O KASSIM ABDI, Miaka 38, Mkazi wa Temeke Mikoroshini ambaye anatuhumiwa kwa kutoa makontena 329 kwenye bandari kavu ya AZAM (AZAM ICD) bila kulipia kodi anayetafutwa na jeshi hilo pia ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni za “JAS EXPRESS FREIGHT LTD” na “XL CLEARING AND FOWARDING Co. LTD” ambazo zote zilitumika kutoa makontena hayo. Ameonyesha picha ya mtuhumiwa huyo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.

Makampuni 26 yamekaidi agizo la Rais John Magufuli alilowataka wafanyabiashara wote waliokwepa kodi kwenye Makontena 326 yaliobainika kupotea bandarini walipe kodi ndani siku saba.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Hata hivyo ni Makampuni 6 ndio waliolitii agizo la magufuli baada ya kulipa kodi iliyokadiliwa  pamoja na Faini ambazo ni Bilioni 10.

Vilevile Makampuni 16 yamelipa kodi  nusu tu tofauti na ile iliyokadiliwa,ambapo siku ya leo ndio siku ya mwisho toka siku aliyosema  Rais Magufuli kuwa ndani ya siku saba wawe wamelipa kodi hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mchana kwenye Makao ya jeshi la polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Meneja wa Huduma na elimu kwa mlipa kodi kutoka wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Diana Masalla huku akiambata na Kamishna wa Kanda Maalum ya Polisi Suleiman Kova ,

Amesema  mpaka leo saa kumi jioni ni makampuni sita tu ndio yaliyolipa kodi hiyo huku mengine 16 yakilipa nusu ya madai ya kodi,huku Makampuni 26 yakishindwa kulipa kodi iliyotakiwa pamoja na Faini ya kukwepa kodi.
“Agizo la Rais magufuli ndio mwisho wake leo saa kumi jioni,lakini wafanyabiashara wenye Makampuni wamekaidi agizo hilo,kwahiyo kama TRA hatuna chengine cha kufanya hapo tunaiachia mamlaka ya sheria kuchukua hatua zaidi”amesema Bi Massala.
Bi Masalla ametaja makadilio ya kodi  ambayo TRA ilifanya kwenye Makontena 326 yaliogunduliwa na Waziri mkuu wiki iliyopita pale alipofanya ziara ya kushtukiza kwenye Bandari ya Dar es Salaam ni Bilioni 28 ambazo zilikuwa zimepotea baada ya wafanyabiashara hao walikuwa wanataka kukwepa kodi.

Kwa Upande wa Kamisha Kova amewaambia wanahabari kuwa Jeshi la Polisi linamtafuta  Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya REGIONAL CARGO SERVICES LTD,ABDULKADIR S/O KASSIM ABDI, Miaka 38, Mkazi wa Temeke Mikoroshini ambaye anatuhumiwa kwa kutoa makontena 329 kwenye bandari kavu ya AZAM (AZAM ICD) bila kulipia kodi .

Kamishna Kova amedai kuwa anayetafutwa na jeshi hilo pia ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni za “JAS EXPRESS FREIGHT LTD” na “XL CLEARING AND FOWARDING Co. LTD” ambazo zote zilitumika kutoa makontena hayo.
Amesema Mwananchi atakayefanikisha kukamatwa kwa mtu huyo (pichani) zawadi nono ya milioni 20 itatolewa kwa atakayefanikisha kutiwa nguvuni.


Hata hivyo,Jeshi hilo pia linawashikilia watuhumiwa 40 ambao wanahojiwa kwa tuhuma za kula njama na kuikosesha serikali mapato. Uchunguzi unafanywa kwa pamoja na maafisa wa Jeshi la Polisi na Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kwa lengo la kubaini jinsi ambavyo makontena 329 na mengine 2489 yalivyotolewa bandarini kinyume cha taratibu.



Kati ya hao, watuhumiwa 26 ni watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)na watumishi 03 kutoka Bandari kavu (ICD) YA AZAM wanatuhumiwa kuhusika na upotevu wa makontena 329. Aidha, watuhumiwa 11 ambao ni watumishi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)  kwa kuhusika na upotevu wa makontena 2489.



Kamisha Kova amesma uchunguzi unaoendelea pia unahusisha kupitia kumbukumbu mbalimbali na kadhia za forodha ili kubaini mtindo uliotumika na kuwabaini wote waliohusika katika mchakato huo. Makontena 329 yaligundulika kukosekana kwenye ICD ya AZAM kuanzia mwezi Julai hadi Novemba 2015, wakati  makontena  2489 yaligundulika kutolewa Bandarini kuanzia Mwezi Machi mpaka Septemba, Mwaka 2014   kinyume cha taratibu kwa lengo la kukwepa kodi na ushuru. 





Uchunguzi bado unaendelea ili kuwabaini wote wanaohusika na hatimaye majalada ya kesi yatapelekwa kwa mwanasheria wa serikali ili watuhumiwa watakaobainika kuhusika na makosa mbalimbali wafikishwe mahakamani 

Hakuna maoni