Zinazobamba

MSANII KALAPINA ACHARUKIA UBUNGE WAKE KINONDONI,AIBUKA NA KUSEMA KAHUJUMIWA,SOMA HAPO KUJUA

Aliyekuwa Mgombea wa Ubunge Jimbo la KinondoniKalama Masud(Kalapina)akizungumza na waandishi
Habari leo jijini Dar es Salaa akipinga matokeo ya Ubunge 
ALIYEKUWA mgombea Mbunge katika Jimbo la Kinondoni kwa Tiketi ya Chama cha ACT-Wazalendo,Kalama Masoud(Kalapina)ameibuka na kuyapinga matokeo.Anaadika KAROLI VINSENT endelea nay.
     Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Kalapina amesema Matokeo yaliyompa ushindi mgombea wa chama cha wananchi CUF ambaye alikuwa naungwa na vyama vinavyoundwa UKAWA,Abdul Mtulia yalikuwa yamesheneni dosari lukuki .
       Amesema katika kata 19 zilizopo katika Jimbo hilo matokeo yake hayakujumlishwa baada mawakala wake kudai walitishiwa na mawakala wa Ukawa na kulazimika kuacha kusimamia vituo hivo.
      “ Yaani mawakala wangu walitishwa na mawakala wa UKAWA,mapaka wakalazimika kuacha kusimamia vituo,  naamini kuondoka kwa mawakala hawa ndio kura zangu za ubunge ndio zikikaibiwa,”
Wanahabari wakimsikiliza kwa makani msanii kalapina

Ameyataja maeneo ambayo amedai mawakala wake walitishiwa ni Kata ya kijitonyama,Tandale,ndugupi pamoja na Kigogo,
     Hata hivyo, Kalapina amesema baada ya kubaini kasoro hizo alilazimika kugomea kusaini karatasi ya wagombea,
      Pamoja na hayo Kalapina amesema hatua iliyobaki sahivi kwake ni kwenda kufungua kesi mahakamani ya kupinga matokeo hayo.

“Lazima niende mahakamani ambapo ndio sehemu pekee ya kupata haki,kwahiyo jumatatu au jumanne ijayo nakwenda kufungua kesi mahakamani ili nipate haki yangu ya msingi kwene jimbo langu la kinondoni.”



No comments