Zinazobamba

DC MAKONDA AJA NA HICHI KINONDONI,SOMA HAPO KUJUA

Pichani ni Mkuu wa wilaya ya Kinondoni DC Mkonda akizungumza na waandishi wa habari

KATIKA kuhakikisha suala la urasimu katika mahakama zilizopo wilaya ya kinondoni linamalizika,mkuu wa wilaya hiyo Paul Makonda ameunda kamati ya maadili ya mahakimu katika wilaya yake.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar Es salaam,Makonda amesema kamati hiyo itasaidia kuondoa kero wanazipata wakazi wa kinondoni kwenye mahakama za wilaya yake.
Amesema mara kwa mara kumekuwa na malamiko kutoka kwa wananch kuwa kumekuwa na ukimkwaji wa haki ikiwemo Kutolewa lugha mbaya kutoka kwa Mahakimu na kucheleweshwa kwa makusudi hukumu za kesi,
   Ambapo amedai kuanzishwa kwa kamati hii itawasiadia wakazi wa kinondoni ambao wanakumbana na matatizo hayo kufika kwenye ofisi ya yake na kukutana na Kamati yake hiyo na kueleza kero hizo ambapo kamati hiyo itakuwa na jukumu la kutafuta haki kwa wananchi.
Makonda amewataja  wajumbe wa kamati hiyo ni Paul Mkonda,Celestine Onditi ambaye ni Katibu Tawala wilaya ya Kinondoni,Frank Mushi Hakimu mkazi mfawidhi wilaya ya kinondoni,Devota Kisoka,Hakimu wa kisutu ambaye mjumbe wa kuteuliwa na Jaji mkazi,
Wengine ni Rose Kangwa aliyekuwa Jakimu Mkazi mahakama ya wilaya ya temeke ambaye amehamishiwa kigoma,Dr Richard Kasungu mjumbe wa kuteuliwa
Hata hivyo Makonda amesema Kamati hiyo itakuwa na majukumu ya kupokea malalamiko yanayowasilishwa na wananchi kuhusu mahakama zote zilizopo wilayani hapo,

Pili,kufanya uchunguzi wa maoni ya katika mwenendo wa mahakama.

No comments