Zinazobamba

KIKWETE AJIABISHA MEDANI YA KIMATAIFA,UBABE UNAOFANYIKA ZANZIBAR WAZIDI MWEKA MSALABANI,SOMA HAPO KUJUA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete

MGOGORO unaendelea sahivi visiwani Zanzibar umeanza kumwaibisha Rais anayemaliza mda wake Jakaya Kikwete kwenye medani za kimataifa baada ya kuonekana sio mtetezi wa demokrasia.Mtandao huu umebaini.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
     Duru zinasema kitendo cha Rais Kikwete kumfumbia macho mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar,ZEC,bwana  bwana  Jecha Salim Jesha kuvunja katiba baada ya kufuta uchaguzi wote na kutangaza kufanyika tena ndani ya siku 90.
         Jecha alitangaza kuufuta uchaguzi huo wiki iliyopita kwa madai ya uchaguzi huo kutawaliwa na dosari ambazo anazodai zimepelekea uchaguzi huo kutokuwa na haki.
      Licha ya kufuta uchaguzi huo,jecha ameonekana kufanya maamuzi ya kurupuka kutokana na kutokuwa na ruhusa kwenye katiba yeyote ambayo inampa mamlaka ya kufanya hivyo,
      Taarifa kutoka Ubarozi wa Marekani ulioko nchini zinasema kitendo cha Rais Kikwete kunyamazia au kumfumbia macho Jecha kinazidi mweka msarabani Kikwete baada ya kuonekana ameshindwa kusimamia demokrasia ya kweli.
       Rais Kikwete ambaye amekuwa akijatamba kwenye medani ya kimataifa kwamba ni mtu wa kujali demokrasia lakini kwa sasa ameshajichafulia kimataifa kwa kuonekana sio mtu wa demokrasia.
        Akizungumza na Fullhabari.blog mwanafunzi wa shahada ya pili ya sayansi ya siasa kutoka chuo kikuu huria cha Tanznaia,Erick Kileo amesema ni kitendo cha Rais Kikwete kumfumbia macho Jecha kwa kumwacha anakiuka katiba ya nchi ni jambo linaloweza kuleta machafuko makubwa Zanzibar.
         “Ujue nyinyi mnafikili Jambo hili ni la Mchezo,maana damu itakapomwagika Zanzibar,hakuna atakayepona kati ya huyo Kikwete na Jecha wake,kwani jambo hili ni baya zaidi haiwezekana mtu mmoja tu kama jecha anakiuka Katiba ya nchi leo Msimamizi wa Katiba ambaye ni Rais Kikwete anamnyamazia tu”
Kuchafuka huko kwa Kikwete kwenye medani ya kimataifa kunakuja ikiwa ni siku tano toka nchi jumuiya ya ulaya kulaani vikali kitendo cha Jecha kufuta uchaguzi huo.
Kwa mujibu wa taarifa kwwa vyombo vya habari zinasema uchaguzi ulifanyika kwa haki na demokrasia ilikuwepo jambo la kushangaza wanashangaa mwenyekiti huyo kufuta uchaguzi huo.
Taarifa hiyo inasema Jecha hana mamlaka ya Kikatiba yeyote kufanya hivyo,huku wakimwamulu aendelea kutangaza matokeo yaliobakia.
Mbali na nchi za Ulaya kulaani vikali “Ubakaji” huo wa Demokrasia teyari  nchi jirani zikiwa zimeshangazwa na kitendo cha Jecha kufuta uchaguzi huo kwa kusema ni jambo la hatari linaloweza kuleta machafuko kama yaliyotokea nchini Kenya.


No comments