WABUNGE WAMNANGA KIKWETE,NI KUHUSU RIPOTI YA TOKOMEZA,SOMA HAPO KUJUA
Baadhi ya athari za Operesheni Tokomeza, askari wakiwadhibu raia |
BUNGE limeitaka Serikali iweke hadharani
ripoti ya Tume ya kimahakama iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete kuchunguza
kilichojiri wakati wa Operesheni Tokomeza. Anaandika Dany Tibason …(endelea).
Akiwasilisha maoni na mapendekezo ya
Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira kwa mwaka wa fedha wa 2015/16,
Mwenyekiti wa kamati hiyo, James Lembeli, amesema “ripoti hiyo tayari
imekabidhiwa kwa Rais na baadhi ya matokeo yake yametangazwa ikiwa ni pamoja na
kuwasafisha mawaziri waliojiuzulu kwa kashfa hiyo.”
Amesema kuwa taarifa
hiyo imewapa maswali makubwa wananchi kwa kuwa ripoti ya kamati ya Bunge
iliyochunguza sakata hilo haikuwatia hatiani mawaziri hao bali waliwajibika kwa
makosa yaliyofanywa na maofisa waliokuwa wanawasimamia.
“Serikali iweke
hadharani ili ripoti iseme ni nini kuhusu wananchi waliuawa, kuteswa, kuporwa
mifugo yao au mifugo hiyo kupigwa risasi. Ni busara kwa serikali kuweka
hadharani ripoti hiyo ili Watanzania waamini kama haki imetendeka,” amesema.
Lembeli amefafanua
kuwa, kamati yake ilikutana mara mbili na kushindwa kujadili taarifa ya Wizara
ya Maliasili na Utalii baada ya kubaini kuwa wizara haikuwa imetekeleza ushauri
wa kamati kuhusu masuala yenye manufaa kwa taifa na haikuweza kutoa sababu za
msingi za kutokutekeleza ushauri huo.
Pia, amemlalamikia
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu kuwa amekuwa akikiuka ushauri
wao, kwamba kamati ilishauri na Bunge likaridhia kwamba mfumo wa ungiaji wa
wageni hifadhini wa mara moja (Single Entry) uendelee kutumika katika hifadhi
za Taifa na Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro.
“Kinyume chake,
wizara iliagiza kutumika kwa mfumo wa uingiaji wa wageni hifadhini zaidi ya
mara moja (Double Entry), hivyo basi hizo taasisi mbili kupoteza mapato
makubwa. Kamati inajiuliza uamuzi huo wa wizara ni kwa manufaa ya nani,”
amehoji.
Amesema kutokana na
hali hiyo, takwimu zinaonesha kwa kipindi cha miezi kumi yaani Julai 2014 hadi
Machi 2015, hifadhi ya Serengeti na hifadhi ya Ziwa Manyara zilipoteza zaidi ya
Sh.1.4 biloni.
Lembeli ameongeza
kuwa wizara kulazimisha mfumo wa uingiaji wa wageni hifadhini zaidi ya mara
moja, kamati inahoji kuna maslahi gani waziri kutetea mfumo ambao unaipotezea
serikali mapato.
Amefafanua kuwa kamati
pamoja na Bunge walishauri waziri atekeleze hukumu ya Mahakama kuu kanda ya
Arusha iliyomtaka kutangaza katika gazeti la Serikali tozo mpya zitakazotumika
katika mahoteli yaliyo ndani ya hifadhi ya Ngorongoro ili zianze kutumika mara
moja.
Kwamba, kutokana na ucheleweshwaji wa kutumika kwa tozo mpya kama
ilivyoamriwa na mahakama, Serikali imepoteza Sh. 3 bilioni hadi kufikia 15
Machi mwaka huu.
“Kutokana na hali
hiyo, kamati inamtaka waziri kulieleza Bunge ni nini kilimfanya akaidi
kutekeleza hukumu iliyokuwa na maslahi kwa taifa. Kamati inashangazwa na hali
ya serikali kulalamika kuwa makusanyo yake ya ndani ni madogo wakati serikali
hiyo hiyo inafanya vitendo vya kujikosesha mapato,” amehoji.
Ujangili wa tembo
Lembeli ameliambia
Bunge kuwa, kwa sasa ujangili wa tembo umekuwa janga la kitaifa.
Amesema ni ukweli usiofichika kwamba tembo sio kwamba wanauwawa
bali kwa sasa tembo hao wanateketezwa.
Amesema kwa mujibu wa
tafiti zilizofanywa na taasisi ya utafiti wa wanyamapori nchini (Tawiri 2011),
zinazoshabihiana na utafiti wa kimataifa, zinaonesha kwamba tembo wasiopungua
30 wanauwawa kwa siku moja na kwa mwezi wanauwawa 850 ambapo kwa mwaka tembo 10,000
wanauwawa.
Lembeli amefafanua
kuwa, kutokana na kasi kubwa ya kuuwawa kwa tembo, taarifa za kitaalam kutoka
Tawiri zinadhibitisha kwamba idadi ya tembo imepungua kutoka 109,000 mwaka 2009
na kufikia chini ya 70,000 mwaka 2012.
Chanzo ni mwanahalisi oline
Hakuna maoni
Chapisha Maoni