Zinazobamba

TAARIFA MUHIMU KUHUSU ACT-WAZALENDO,BONYEZA HAPO KUJUA

PICHANI NI KATIBU MKUU WA ACT-WAZALENDO
PICHA NA MAKTABA

CHAMA cha Siasa cha ACT-Wazalendo kimewaomba Wanachama wa Chama hicho,wapenzi pamoja Watanzania wapenda mabadiliko kukichangia pesa  kwa hali na mali, ili kiweze kuanza Ziara yake ya pili  mikoani ya   kutoa elimu kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi katika uandikisha kwenye Daftari la wapiga kura.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
      Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho  Samson Mwigamba wakati akizungumza na Mtandao huu ambapo amesema kutokana na umuhimu wa suala Daftari la wapiga kura ni wazi chama hicho kimepanga kuwahamasisha watanzania kujitokeza kwa wingi ili kutimiza jukumu lao la msingi Kikatiba.
         Mwigamba pamoja na hayo amebainisha kuwa ili chama hicho kifanikisha ziara hiyo kinawaomba watu mbalimbali nchini kichangia Fedha za kununua Mafuta,kukodisha Magari pamoja na Fedha za kujikimu kwa Viongozi wa ACT-Wazalendo watakapokuwa wakitoa Elimu hiyo.
         Aidha,Mwigamba alizitaja njia za kuchangia pesa ambapo ni njia mbili ambazo ni kwa MPESA  namba 0763463740 jina ni ACT POLITICAL au kwa Tigo pesa pia ni kwa namba 0715 784670 kwa jina la (ACT –TANZANIA).

      Mbali na njia hiyo za simu pia Mwigamba amesema hata kwa njia ya Benki ya NMB wanaweza kuchagia kupitia Akaunt NO-22610004083 Jina la ACT –Tanzania.

No comments