Zinazobamba

MWANDISHI KUBENEA AWACHUKIZA VIONGOZI ACT-WAZALENDO,MWIGAMBA ASEMA HAYA

Pichani ni KATIBU MKUU WA CHAMA CHA ACT-WAZALENDOSAMSON MWIGAMBA PICHA NA MAKTABA

KILE kinachoonekana ni kama Viongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo wamesindwa kuvumilia juu ya Makala Mfululizo zinazoandikwa na Mwandishi Saed kubenea kwenye Gazeti la Mawio kuhusu mwenendo chama hicho.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
            Baada ya Hivi sasa viongozi wa Chama hicho kichanga cha siasa nchini kuibuka na kusema uvumilivu utafikia mwisho na kutishia kumfikisha Mahakamani Mmiliki wa Gazeti hilo pamoja na Mhariri wake.
           Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Chama hicho Samson Mwigamba wakati akizungumza na Mwandishi wa Mtandao huu kwenye Semina iliyoaandaliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC) iliyowakutanisha wanasiasa mbali mbali wa vyama vyote vya Siasa nchini kujadili mambo mbali mbali kuelekea uchaguzi Mkuu hapo baadae mwaka huu ambapo-
       Mwigamba akizungumza kwa uchungu amesema kwa sasa viongozi wa chama hicho wanasikitishwa na Uandishi ambao wanadai ni wa kutumiwa na watu wenye mapenzi mabaya na ACT-Wazalendo kwa kuandika Makala zilizojaa uwongo.
      “Hivi ule ni uwandishi wa aina gani,maana inasikitisha kuona  miezi zaidi ya mitatu mwandishi na Mhariri wanaandika habari moja tu yaani kila siku na ACT-Wazalendo tena kwa mabaya yaani hawajawai kuandika makala zinazohusu mazuri,wao ni mabaya tu na hayo mabaya ni ya uongo hayana ukweli ,lakini uvumilivu unamwisho  nakwaambia tutachoka na sisi tutakwenda hata mbele ya Sheria”amesema Mwigamba.
Mwigamba ambaye kabla ya kuwa ACT-Wazalendo alikuwa kiongozi wa Chadema Mkoani Arusha na alifukuzwa Viongozi wa chama hicho kwa madai ya kuandaa mipango ya kuhujumu chama hicho Kikuu cha Upinzania nchini.

       Kuibuka huko kwa Mwigamba kunakuja ikiwa umepita mwezi mmoja  baada ya Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo nchini Zitto Kabwe kumtuhumu Mmiliki wa Gazeti la Mawio ambaye Kabwe anasema ndio mmilikiwa Mtandao wa Mwanahalisi.oline kuandika Habari ambazo Zitto anazidi dai kuwa zilikuwa zina lengo la kumgombanisha na Mwenyekiti wa IPP Bwana Mengi.

No comments