Zinazobamba

MACHAFUKO NCHINI BURUNDI TANZANIA YAANZA KUPATA ATHARI ZAKE,SOMA HPO KUJUA




ATHARI za machafuko ya kisiasa yanayoendelea nchini Burundi yamenza kuigusa Tanzania,baada ya wakimbiza wanaokimbia machafuko hayo  kuja Mkoani Kigoma wamesebabisha kuibuka ugonjwa mkubwa wa kipindupindu na kusababisha vifo vya watu 10 mpaka sasa.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
       Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Afya  Dkt.  Steven Kabwe  Wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo amesema Wizara yake kwa kushirikiana na Ofisi ya Mganga Mkuu mkoani Kigoma  pamoja na mashirika mbali mbali ya Kimataifa ya kuwahudumia Wakimbizi wamethibitisha kutokea na Vifo hivyo ambapo vyote vimetokana na Ugonjwa wa Kipindupindu.
“Kwa sasa tumethibitisha pasipo shaka watu 10 wamekufa kutokana na Ugonjwa wa kipindupindu na baada ya kufanya uchunguzi ambao tulishirikiana na mashirika ya Kimataifa tumebaini sehemu kubwa ya Ugonjwa huu umetokana na ujio wa wakimbizi kutoka nchini Burundi”amesema
Kwa Mujibu wa Naibu Waziri Kabwe amesema Mpaka jana Teyari walikuwa wameshawapokea wakimbizi Laki mbili kutokea Burundi ambapo anasema kutokana na Ufinyu wa maeneo ikiwemo matumizi ya Maji pamoja na uchache wa huduma za choo ndio imekuwa miongoni mwa sababu ya kuibuka Ugonjwa huo.
Pamoja na hayo amebainisha kuwa kwa sasa  hatua ambazo Serikali imechukua za haraka ni kuwapeleka madaktari pamoja na huduma mbali mbali za kibanadamu ili kuweza kuokoa Tatizo hilo kubwa.

         Aidha,Muheshimiwa Kabwe akawataka Waganga wakuu wa mikoa nchi nzima pamoja na Wananchi kuchukua tahadhari ikiwemo kuweka maeneo safi.

No comments