HABARI KUBWA LEO.WAZIRI MAGUFULI AMTIA KIWEWE LOWASSA,KAMBI YAKE YAJITOSA KUPAMBANA,SOMA HAPO KUJUA
Pichani ni Edward Lowassa |
SIKU moja kupita
baada Waziri wa Ujenzi Dk John Pombe Magufuli kutangaza Rasmi kujitosa kwenye
nafasi ya Urais ndani ya chama cha Mapinduzi CCM,kunatajwa kuiweka kiwewe kambi
ya Edward Lowassa ambaye anautaka Urais
kwa udi na Uvumba ndani ya Chama hicho,Mtandao huu umebaini.Anaandika KAROLI
VINSENT endelea nayo.
Dk. Magufuli, mmoja wa
mawaziri ambao kwa muda mrefu wamehusishwa kwenye kinyang’anyiro cha nafasi
hiyo, alisema anaingia kwenye mchuano huo akiwa na sifa zote stahiki za kupiga
na kupigiwa kura.
Alitangaza azma yake nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, muda mfupi baada ya kumalizika kipindi cha maswali na majibu bungeni, jana asubuhi.
Taarifa za kuaminika ambazo mtandao huu umezipata kutoka ndani ya Kambi ya Lowassa ambaye ni Waziri mkuu aliyejiuzulu kutokana na Kashfa ya Ufisadi kwenye Kampuni Tata ya Richmound zinasema kwa sasa kambi hiyo imejipanga kuhakikisha kumwandalia mipango ya Kumchafua kwa Wajumbe wa Halmashauri kuu NEC ili jina lake lisipite.
Alitangaza azma yake nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, muda mfupi baada ya kumalizika kipindi cha maswali na majibu bungeni, jana asubuhi.
Taarifa za kuaminika ambazo mtandao huu umezipata kutoka ndani ya Kambi ya Lowassa ambaye ni Waziri mkuu aliyejiuzulu kutokana na Kashfa ya Ufisadi kwenye Kampuni Tata ya Richmound zinasema kwa sasa kambi hiyo imejipanga kuhakikisha kumwandalia mipango ya Kumchafua kwa Wajumbe wa Halmashauri kuu NEC ili jina lake lisipite.
Lowassa
ambaye kesho anatarajia kutangaza nia ya kuwania nafasi ya Urais ndani ya Chama
hicho , mkoani Arusha kwenye Uwanja Sheikh Aman Abed Karume na kurushwa
moja kwa moja (Live) na Luninga zaidi ya tatu sanjari na Redio zaidi ya tano,
Mbali
na kutangaza huko nia yake ya Urais ndani ya chama chake pia Lowassa anatajwa
pia kuliweka bayana suala na Mkataba wa Kinyonyaji wa Richmound.
Akizungumza kwa sharti la kutaja jina
lake Mjumbe wa Kamati wa Kambi ya Lowassa amesema kutangaza nia kwa Waziri Magufuli kumeleta
msuguano ndani ya kambi hiyo.
“Sikiliza ndugu sahivi kambi ya mzee (Lowassa) imepata
mtikisiko mkubwa sana baada ya kusikia
nae magufuli anautaka Urais kiukweli
mambo yatakuwa magumu”amesema Mjumbe huyo.
Sababu ambayo inatajwa na wajumbe hao
kwa Magufuli inatokana na hazi aliyokuwa nayo kwenye jamii ikiwemo kasi yake ya
aliyoonyesha ndani ya wizara alizoziongoza ikiwemo Wizara anayongoza sahivi ya Wizara ya Ujenzi.
“Huyu bwana
kiutendaji yupo vizuri sana,tena anaonekana ni mtu wa maamuzi mazuri,harafu
anauchungu na watanzania mbali na hivyo pia hata watanzania wanamkubali kwani
ana viashilia vya udikteta na Taifa linaitaji mtu kama huyo na ndio maana kambi
ya Lowassa inakuwa na wasi wasi”ameeleza mchambuzi wa siasa kutoka Dar es
salaam.
WAJUMBE WA NEC WANENA.
Wajumbe wa
Halmashauri kuu ya CCM (NEC)waliozungumza na Mtandao huu wameoneshwa kuchukizwa
na kitendo cha Lowassa kuunda “utatu mtakatifu” na watu ambao wanatajwa
kuhusika kwenye kashfa mbali mbali za Ufisadi.
“Mimi
mwenyewe nilikuwa mtu wa lowassa ila kwa sasa nimekata tama na kusema huyu mtu
afai ndani ya nchi hii,leo nashangaa sana anashirikiana na watu mafisadi kama
wakina Rostam,Chenge,Karamagi,watu ambao wameliangamiza Taifa hili kwa ufisadi
wao,harafu leo ndio watu wake wewe unategemea nini”amesema Mjumbe wa NEC kutoka
mkoani Mbeya.
Dk. Magufuli, amekuwa mbunge tangu mwaka 1995 aliyasema
hayo Baada ya kuulizwa kama ana mpango huo, mara moja alisema: “Swali hili
nimeulizwa mara nyingi. Mara zote nimekataa kulijibu kwa sababu chama chetu
(CCM) kuna utaratibu wake wa namna ya kuomba nafasi ya uongozi. Muda ulikuwa
haujawadia.
“Lakini utakumbuka wiki hii hapa hapa Dodoma, vikao vya juu vya chama chetu vimetoa ratiba kwa wanaotaka kuwania nafasi mbalimbali kujitokeza.
“Kwa maana hiyo sasa niko huru kujibu swali lako kwa kusema rasmi ‘nitagombea urais’. Nafanya hivyo kwa sababu naamini ninazo sifa za kuchagua na kuchaguliwa kama mwanachama wa CCM kwa nafasi yoyote inayojitokeza kulingana na Katiba ya chama chetu na pia Katiba ya nchi,” alisema Dk. Magufuli.
Alisema siku ya kuchukua fomu ataitangaza baadaye pindi akishakamilisha taratibu za namna ya kuanika hadharani mambo anayokusudia kuyatekeleza endapo wana CCM watampa ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama hicho.
“Lakini utakumbuka wiki hii hapa hapa Dodoma, vikao vya juu vya chama chetu vimetoa ratiba kwa wanaotaka kuwania nafasi mbalimbali kujitokeza.
“Kwa maana hiyo sasa niko huru kujibu swali lako kwa kusema rasmi ‘nitagombea urais’. Nafanya hivyo kwa sababu naamini ninazo sifa za kuchagua na kuchaguliwa kama mwanachama wa CCM kwa nafasi yoyote inayojitokeza kulingana na Katiba ya chama chetu na pia Katiba ya nchi,” alisema Dk. Magufuli.
Alisema siku ya kuchukua fomu ataitangaza baadaye pindi akishakamilisha taratibu za namna ya kuanika hadharani mambo anayokusudia kuyatekeleza endapo wana CCM watampa ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama hicho.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni