Zinazobamba

HABARI KUBWA LEO-LOWASSA BASI TENA,MAWAZIRI WA KIKWETE WAMMALIZA,KUTEGEMEA MIUJIZA,SOMA HAPO KUJUA


UWEZEKANO wa Edward Lowassa kutaka kugombea  Urais ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) umefikia mwisho .Mtandao huu umedokezwa.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
        Taarifa za kuaminika ambazo mtandao huu umezipata kutoka ndani ya CCM zinasema mpango wa kumzuia Lowassa unasukwa kwa Ustadi mkubwa na Waziri mmoja Mwandamizi wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete ambapo anasema  “huyu lowassa anapoteza mda tu na tushaweka mipango kwamba Jina lake tutalikata katika hatua za awali za kinyang’snyiro cha Urais”
        Kwa mujubu wa Mtoa taarifa huyo kwa Mtandao huu amesema Lowassa ambaye ni Waziri mkuu   aliyejiuzulu kwa Kashfa ya Ufisadi kwenye Kampuni Tata ya Richmound  ambapo inaelezwa kwamba katika mkutano wa Halmashauri kuu (NEC) na Kamati kuu uliopangwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii utakuwa na kazi ya  kuliondoa jina kabla ya muda wa kuchukua Fomu kuwadia.
       Kwa mujibu wa Mipango hiyo inayosukwa na Waziri huyo Mwandamizi umejikita kwenye Hoja ya kwamba Lowassa ameanza kampeni mapema kabla ya chama chake akijatoa mwongozo,pili ni kujenga mtandao ndani ya chama na kujikita kupanga safu za uongozi jambo ambalo waziri huyo anasema ni kukidhofisha Chama hicho.
       Mbali na madai hayo pia Lowassa anatuhumiwa kuzunguka nchi nzima  kufanya Mikutano na Baadhi ya wajumbe wa (NEC ) ,wenyeviti wa Mikoa na makada mbalimbali ngazi za kata na kuwapa pesa ili wamshawishi mwenye Mbio zake za Urais.
        Chanzo hicho kinadai Lowassa ambaye ni Mbunge wa Munduli alikuta na wajumbe wa NEC na baadhi ya wenyekiti wa mkoa kanda ya ziwa Viktoria pamoja viongozi wa madhehebu ya kidini kati ya mei 2013 na januari mwaka jana.
        Mpango huo wa kumkata Jina unakuja ikiwa Teyari Lowassa mwenyewe ameyakataza makundi mbali mbali ya kijamii waliokuwa wanakwenda kumshawishi kwa kusema chama chake kimekataza na kuwataka kusubili kwanza.
        Lowassa ambaye pia ni Miongoni mwa Makada wa Chama hicho ambao wanataka Urais Kwa udi na Uvumba ambapo kwa Mujibu wa Wapambe wake wanasema wapo teyari kumuingiza ikulu kwa Machela ya kubeba wagonjwa.
        Taarifa hizo zinakuja ikiwa teyali chama hicho kwa kupitia Katibu wake wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauya kutangaza  ratiba ya Vikao vya NEC na CC vilivyopangwa kufanyika Mjini Dodoma Kuanzia 20 mei hadi 22,ambapo pamoja na mambo mengine ni vitajadili na kuhitimisha suala la adhabu la makada wake sita wakiongozwa na Lowassa ambao wote kwa pamoja wanatuhumiwa kuanza kampeni mapema ya kutaka Urais.
    Mbali na Lowassa makada wengine waotarajiwa kujadiliwa kwenye Kikao hicho ni Waziri mkuu wa awamu ya tatu Frederick Sumaye, Waziri wa Ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe,Waziri wa Kilimo ,chakula na Ushirika Steven Wasira,Naibu waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia January Makamba pamoja na Mjumbe wa NEC ambaye amesemamishwa  kutokana na Ufisadi wa ESROW William Ngeleja.
   Kwa mujibu wa Mtoa taarifa wetu amesema Mikutano hiyo mbali ya kuwajadili makada hao pia itatoa Ratiba ya na utaratibu wa kuchua fomu za kugombea nafasi mbali mbali.
        Taarifa za Vikao hivyo zinakuja ikiwi ni wiki moja kupita baada ya Mtandao huu kufichua mipango ambayo inapangwa ya kwenda kuvuruga vikao hivyo kabla ya kukutana na ‘kuyachinja’ majina hayo.
    “Kwa sasa waziri (jina tunalihifadhi) ameshamkabidhi majukumu yote mwenyekiti wa CCM (bara) Philip Mangula kulikata kabisa jina lake na kuwa na  hoja zinamshiko ambazo watatumia kuliondoa jina la lowassa”amesema mtoa taarifa huyo
      Sanjari na hayo pia kwa sasa Chama hicho kikongwe barani Afrika kimepanga kubadili mfumo wake wa uchukuaji fomu na kuweka mfumo wa mpya  wa uchukuaji ambao unawaradhimu  makada  wa chama hicho kutakiwa kujitangaza kupitia vyombo vya Habari lengo  ni kuwakaba makada wake.

        Mpango wa Kulikata jina la lowassa unasukwa kwa Ustadi mkubwa na wa Ajabu na baadhi ya Mawaziri wa Rais Kikwete pamoja na Idara ya Usalama wa Taifa ambao kwa mujibu ya wao wanasema mipango hiyo imebarikiwa na nguvu zote ma Rais Kikwete mwenyewe.

No comments