Zinazobamba

TLS, IBA WAWAKUTANISHA WANASHERIA PANDE ZOTE DUNIA KUJADILI RASILIMALI YA MADINI, MKUTANO HUO UTATOA SULUHUSU YA MIKATA MIBOVU

WAKILI Daniel;WEL WEL akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari kuhusu mkutano mkubwa wa wanasheria utakaofanyiaka hivi karibuni katika ukumbi wa mwl. Nyerere. Welwel ameutaja mkutano huo kama mkutano wa ukombozi ambao utatoa mafumnzo mazuri kwa Waafrika kuhusu fulsa na changamoto za sekta ya madini

Nafanua zaidi, wakili huyo akifafanua zaidi


DARESALAAM
Tanzania kupitia chama cha wanasheria cha Tanganyika law society (TLS) inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa wa aina yake wenye lengo la kujadili fulsa na changamoto za kisheria zinazoikabili sekta ya madini katika bara la Afrika hivi karibuni
Akizungumza na waandishi wa habari mapema hii leo, muandaji wa mkutano huo ambaye pia ni mjumbe wa Tanganyika Law Society Wakili Daniel WEL WEL amesema, mkutano huo umekuja kufuatia kuonekana kwa unyonyaji wa mikataba mbalimbali ya kisheria inayofanywa na wawekezaji katika sekta ya madini
Wakili Wel Wel ameendelea kusema kuwa kwa muda mrefu Tanzania kumekuwa na vilio kuhusiana na mikataba kwa sekta ya madini ,hivyo ujio wa mkutano huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kujua wenzetu katika mabara mengine duniani wanafanya nini mpaka rasilimali zao zinaweza kuwanufaisha,
Naye katibu mkuu wa chama hicho cha (TLS) Wakili Alphonce Gura ametaja Baadhi ya Changamoto ambazo zitaangaliwa kwa kina katika mkutano huo kuwa ni pamoja na zile za kisheria,kiuchumi na za kimazingira ambazo mara nyingi zimekuwa zikiwaathiri wakazi walio karibu na mazingara ya uchimbaji wa madini

Akielezea sababu za chama cha wanasheria duniani (IBA) kukubali kupeleka mkutano huo Tanzania, wakili Gura amesema fulsa hiyo imekuja kufuatia mwenendo mzuri wa ukuaji wa uchumi wa taifa na kuongezeka kwa kasi ya ukuaji wa sekta ya madini hapa nchini
Katika mkutano huo unaotarajiwa kuhudhuriwa na watu mbalimbali toka kila kona ya dunia utahusisha jumla ya washiriki 150 ambao watajadili ni namna gani wanaweza kulisaidia bara la Afrika kuondokana na tatizo la kisheria katika sekta hiyo ya madini, na kwamba mgeni rasmi katika mkutano huo anatarajiwa kuwa Naibu waziri wa nishati na madini
MAGALLI………………PRESS………………..03/09/2014

No comments