MAKAME MBALAWA AZINDUA HUDUMA ZA MATIBABU KWA NJIA YA MTANDAO HUKO bAGAMOYO
| kulia ni Muheshimiwa waziri, Makame Mbalawa na kushoto ni Mkuu wa mfuko wa mawasiliano kwa umma, Eng. Peter Ulanga wakiwa katika mkutano huo |
| Picha ya pamoja ya wadau baada ya kufunguliwa kwa mkutano huo wa siku mbili kuhusu matibabu kwa njia ya mtandao |
Akifungua mkutano huo waziri MBARAWA amesema kuwa huduma ya telemedicine ni muhimu sana kwa wananchhi wa Tanzania,kutokana na ukweli kuwa ni huduma ya haraka na isiyogharimu kwenda umbali mrefu.
Huduma hiyo ambayo iliyofanyiwa majaribio katika hospitali saba nchini imeonyesha mafanikio makubwa na hivyo serikali inafikiria kuziunganisha hospitali zote muhimu za wilaya na mikoa hapa nchini na huduma hiyo.
Akizungumzia jinsi huduma hiyo inavyofanya kazi waziri mbarawa amesema kuwa ni huduma ambayo inatafutwa kama huduma nyingine isipikuwa utofauti wake ni huduma ambayo inapatikana kwa haraka kutokana na kuhusisha mtandao.
Kwa mujibu wa huduma hiyo ni kwamba Daktari anaweza kuwasiliana na Daktari ambaye yupo hosipitali nyingine na kuweza kutoa maelekezo moja kwa moja kwa daktarri husika kwa ajili ya kumhdumia mgonjwa na huuduma kuendelea kama kawaida.
Aidha katika hatua nyingine wizaya yake pamoja na wizara ya afya wamekubaliana na mtandao wa VODACOM TANZANIA kuanza kutoa huduma ya mtandao bure katika hospitali ya taifa muhimbili ikiwa ni jitihada za kurahisisha huduma katika hospitali hiyo
Wkifafanua kuhusu huduma hiyo inavyofanya kazi wataalam mbalimbali toka wizara ya afya na mawasiliano wamesema ni huduma ambao inafanywa kwa njia ya mitambo
"Mama yako mzazi yu mgonjwa mahututi katika hospitali ya Wilaya ya Masasi. Madaktari wamelifahamu tatizo lake lakini hakuna vifaa wala wataalamu wa jinsi ya kumtibu. Anatakiwa ahamishiwe Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako kuna madaktari bingwa na vifaatiba vya uhakika. Hata hivyo safari ya kutoka Masasi hadi Dar Es Salaam, pengine yaweza kupoteza uhai wake.
Lakini usihofu... Tanzania sasa imepata neema baada ya kuwepo kwa huduma ya Tiba kwa njia ya Teknolojia ya habari na mawasiliano, kwa kitaalamu ‘telemedicine’
Telemedicine ni utoaji wa huduma za afya au mbadilishano wa taarifa za kitiba kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano.*
*Mafanikio ya uvumbuzi huu yamesaidia wataalamu wa afya kubaini na kutibu wagonjwa bila kuonana nao uso kwa uso.*
*Kwa kifupi, unaweza ukazungumza na daktari wako na kumweleza vile unavyojisikia, kisha akakuandikia vipimo, na baada ya kumpa majibu ya vipimo hayo kwa njia ya teknolojia pia, atakuandikia dawa au kukupa ushauri wa kitiba.
Pia, Hospitali yenye vifaa na wataalamu wanaweza kuzungumza na madaktari katika hospitali za vijijini na kutoa ushauri wa jinsi ya kumtibu mgonjwa aliye taabani.
Hivi sasa hospitali saba nchini zimeunganishwa katika mradi huo wa Telemedicine ambazo ni Mwananyamala, Amana, Temeke na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH) pamoja na hospitali ya Tumbi, Mkoa wa Pwani.
Mei, 2011 ndiyo wakati ambao Rais Jakaya Kikwete alizindua mradi huu akiwa pamoja na Makamu wa Rais wa India, Dk Manmohan Singh.
Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Modou Gaye anasema teknolojia hii inawezesha madaktari walioko katika Hospitali za Amana, Mwananyamala, Temeke, Tumbi na Bagamoyo kuwasiliana moja kwa moja na madaktari bingwa pamoja na watalaamu wengine walioko Muhimbili katika kujadili, kushauriana na
hatimaye kufanya uamuzi kuhusiana na tiba, uchunguzi wa mgonjwa husika.
Gaye anasema kuwa teknolojia hii itamwezesha mgonjwa aliyeko kati ya ospitali hizo kupata matibabu bila kufika Muhimbili.Anasema kupitia teknolojia hii wataalamu wataweza kuwasiliana katika nyanja za ushauri, vipimo vya uchunguzi mathalan vya radiolojia, vipimo vya uchunguzi vya patholojia, magonjwa ya moyo na mafunzo kwa watalaamu.
Uwepo wa teknolojia hii utawezesha mgonjwa anayehitaji kupata huduma za kibingwa Muhimbili kutibiwa haraka na kwa muda mfupi kuliko ambayo angefuata utaratibu wa rufaa na hivyo kumpunguzia muda wa kukaa hospitalini kwa muda mrefu.
No comments
Post a Comment