MBUNGE MSALITI ANUSURIKA KIPIGO NA WANANCHI,KISA SIASA ZAKE ZA MAJITAKA SOMA HAPA UONE ALIVYONUSULIKA
Pichani ni Mbunge msaliti Said Arfi kutoka Jimbo la Mpanda mjini CHADEMA.
Katika hali ambayo inazidi kupigilia msumari wa
mwisho kwenye maisha yake ya kisiasa, Mbunge wa Mpanda Mjini, Said Arfi
amenusurika kipigo kutoka kwa wananchi wa jimboni kwake baada ya kujitangaza
kwamba yeye ni CCM huku akiibeza Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Tukio hilo lililotokea Jumatatu ya wiki hii eneo la Maridadi mjini
Mpanda limeacha gumzo la aina yake katika viunga vya mji huu huku wananchi
wakionekana kuifikisha ukingoni safari ya kisiasa ya mbunge huyo katika namna
ambayo almanusura ingemgharimu sana.
Tukio lilianza kwa Mbunge Arfi kuitisha mkutano wa hadhara aliosema eti
si wa kisiasa, ambapo meza kuu aliketi na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpanda
anayetokana na CCM
viongozi wengine kadhaa wa CCM, ma-VEO na WEOs wa Mpanda, madiwani
wawili wa CHADEMA ambao wanajulikana ni wasaliti. Wengine walioandamana naye
jukwaani ni viongozi wa CHADEMA waliotimuliwa hivi karibuni kwenye Kamati ya
Utendaji ya CHADEMA kwa makosa ya kufanya kazi za CCM kupitia tawi jipya
liitwalo ACT.
Alipopanda jukwaani tu kuanza kuzungumza wananchi wakamtaka kwanza
awaambie yeye ni chama gani kwa sababu walikuwa hawamwelewi kutokana na
composition ya meza kuu ambayo yeye ndiyo alikuwa ameialika huku akiwaweka
kando kabisa viongozi wa chama kilichomdhamini kupata ubunge ambao ameshindwa
kuwakuwatumikia wananchi.
Baada ya kuombwa aseme yeye ni chama gani, Mzee mzima aka-panic na
kuanza kujibizana na wananchi kwenye mkutano wa hadhara eti ule si mkutano wa
siasa
Makelele yalipozidi akaamua kusema yeye ni gamba yaani CCM. Akawa kama
amechokoza nyuki. Yakaanza makelele ya wananchi wakitaka arudishe kadi ya
CHADEMA pale pale mkutanoni Mzee akazidiwa kabisa
Akazidi kusema mbovu kwamba maeneo yote nchini ambako kuna ‘pipooooz power’
(yaani majimbo yanayoongozwa na wabunge wa CHADEMA) hakuna maendeleo ndiyo
maana yeye amemua kuachana na hiyo pipooooz power kwa sababu anataka maendeleo
jimboni kwake.
Akaenda mbali na kuanza kukandia mchakato wa Katiba Mpya kwa kuuponda
UKAWA akisema yeye si UKAWA na hautambui umoja huo. Akaiponda Tume ya Warioba
akisema haijasema kweli huku akihoji kama kuna mwananchi yeyote anayejua kuwa
Tume imesema ukweli anyooshe mkono. Kufika hapo sasa mkutano ndiyo ukavurugika
kabisa.
Wananchi wakasema hawezi kutuka Tume ya Mabadiliko a Katiba. Hana sifa
za kukandia UKAWA, wala hadhi ya kuhoji kazi nzuri ya Jaji Warioba liyozingatia
maoni ya wananchi.
Akalazimika kufunga mkutano.
Wananchi wakamzingira pale pale, wakisema madam ameshasema yeye ni CCM basi
awaachie pale pale kadi ya CHADEMA aondoke aende zake. Mzee akawa hawezi kutoka
pale.
Shukrani kwa Jeshi la Polisi. Zikafika gari tatu za polisi, mojawapo
ikiwa imejaa FFU kuja kumuokoa. Polisi walipoona mtiti wa wananchi waliokomaa
kwa dhamira moja ‘kubaki’ na kadi ya Arfi, wakalazimika kutumia diplomasia
kuwaomba wananchi wamuachie yule mbunge.
Akaondoka uwanjani kwa ulinzi wa magari matatu ya polisi yeye akiwa
katikati hadi nyumbani ambako pia polisi walilazimika kuweka ulinzi wakijua
kuwa kwa hasira mabazo wananzo wananchi dhidi ya mbunge yule kutokana na
matukio mengine ya nyuma ya usaliti, wangeweza kumfuata hadi nyumbani.
Wakati wananchi wakianza kusambaa, mara akapita mdogo wake na Arfi
aitwaye Nasoro, ambaye wananchi wenye hasira hawakujua kuwa ni mtu wa misimamo
na hayuko na kaka yake katika masuala ya usaliti. Wakamvaa kumaliza hasira
zao.
Bila watu wengine wanaomjua Nasoro kuwa ni mwanachama na mpenzi mkubwa
wa CHADEMA Mpanda kuwahi kumwokoa, tungesema habari yingine muda huu.
Wananchi hao wenye hasira waliamua kwenda kumalizia ghadhabu zao kwenye
Ofisi za CHADEMA Wilaya ya Mpanda wakikumbushia matukio ya Arfi kushirikiana na
MM ‘kuuza’ jimbo kwa Waziri Mkuu na lile la kutupa kadi ya uanachama wakati
akiwa bado Makamu Mwenyekiti wa Chama Taifa.
Kesho yake Jumanne ndipo Arfi akaamua kuukimbia
mji na kukimbilia Dodoma.
No comments
Post a Comment