Zinazobamba

EXCLUSIVE---MCHAKATO WA KATIBA MPYA WAANZA KUMCHAFUA RAIS KIKWETE KIMATAIFA,UJUE KWANINI SOMA HAPA KUJUA



 
pichani ni Rais Jakaya Kikwete picha na Maktba

Na Karoli Vinsent
RAIS Jakaya Kikwete uwenda  akachafuka Kisiasa kwenye Medani za Kimataifa endapo mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya ukikamilika na  katiba mpya kupatikana , bila ya kuwepo wajumbe wanaounda umoja wa katiba ya Wananchi (UKAWA),umetajwa  ndio itakuwa sababu itakayamshusha hadhi Rais Jakaya Kikwete kwenye Medani za Kimataifa,Mtandao huu umebaini.
          Rais Kikwete,ambaye hivi karibuni ambaye amepewa tuzo mbalimbali ikiwemo tuzo aliyopewa  ya Nyota wa Demokrasia  Afrika 2014-Icon of Demokrasia Award winner for 2014 in Africa,
          Tuzo hiyo aliopewa na jarida la the Voice kutokana na michango mbalimbali ya kidemokrasia aliyoionyesha barani humu,ikiwemo jitihada alizozifanya za kutuliza amani nchini Kenya kwenye machafuko ya Kisiasa mwaka 2007,ambapo Rais Kikwete alifanikiwa kutuliza amani nchini Humo.

            Lakini kwa sasa Rais Kikwete ameanza kuchafuka kisiasa kimataifa kwa kitendo chake cha kuharibu mchakato wa upatikanaji katiba mpya,
           Kwa mujibu ya taarifa mbalimbali kutoka kwa mataifa tofauti Duniani zinasema macho na masikio kwenye mataifa mengi  yameelekezewa Tanzania katika kipindi hiki cha Historia cha undikaji wa Katiba ambayo sasa imekuwa na mpasuka mkubwa ambao umesababishwa na Ghiliba za chama chaMapinduzi CCM,kwa kuyapuuzia maoni ya wananchi na kuanza kuingiaza maoni ya chama hicho.
            Na endapo Rais Kikwete ataungana na mafahidhina kutoka chama chake ambao hawapendi upatikanaji wa Katiba mpya na kuzidi kuendelea kushikili bango suala la Serikali mbili na kuyachingia mbali maoni ya Serikali tatu ambayo yaliyotolewa na wananchi kutazidi kushusha  umaharufu wake Kisiasa alioanza kuupata Duniani licha ya yeye kushidwa kuondoa Umasikini.
       Kwa upande wake akilizungumzia hili, Mwanasheria wa Umoja wa Kutetea katiba ya Wananchi UKAWA,Tundu Lissu amesema kwa hali ilivyo basi ni ishara tosha hakuna uharali kuhuhu tuzo anazopewa Rais Kikwete.
        “Ngoja niseme Mataifa makubwa Yanayotunyonya yanatumia mahusiano na Vibaraka kwenye nchi husika  ambazo wanaziibia Fedha kupita uwekezaji kama madini pamoja na Mabenki yao yaliyokuwepo nchini,na wanakuja kutoa shukrani kwa kuwapa Tuzo na kwa hali hii mimi sioni Jipya juu yeye kuchafuka kwenye madeni za kimataifa”alisema Lissu.
     Tundu Lissu ambaye ni Mjumbe pia wa Bunge Maalum la Katiba alizidi kushikilia bango kwamba wao hawatarudi kwenye Bunge hilo Maalum la katiba kutokana na leo kuanza kujionyesha wazi kwamba wanaendeleza mambo yao.
             “Umeona mwenyewe leo wameanza kubadilisha kanuni na wanafanya hivi iliwaendeleze kutunga katiba itakayotokana na Maoni ya chama cha CCM na kuzika maoni ya Wananchi na tunasema sisi hatutoshiriki kwenye jambo hili na hatuwezi kurudu”aliongeza Lissu
        Akizungumzia na Mtandao huu pia, Mchambuzi wa Masula ya Kisiasa kutoka chuo kikuu cha Dodoma Nchini, Seiph Yahaya alisema huu ni wakati wa kumpima kisiasa Rais Kikwete kuhusu uharali wa tuzo anazopewa je zina stahili?
                “Na sasa ni wakati mzuri sana wa kupima Rais jakaya  Kikwete kwenye huu mchakato wa katiba Maana mchakato huu wa katiba ukiendelea hivi pasipo kuwa na upande mmoja wa kisiasa ambao ni UKAWA  unaweza kumchafua sana Rais Kikwete kimataifa kwani inaonekana kwa zile Tuzo alizopewa ni za kiupendeleo”alisema Yahaya
          Yahaya aliongeza na kusema kama Rais aliweze kutuliza Amani nchini Kenya anashindwa vipi kuachana na Ghiliba za chama chake ambazo wanashikilia mfumo wa Serikali mbili ambao utokani na Maoni ya wananchi na kuuacha mfumo wa Serikali tatu uanotokana na Maoni ya Wananchi.
           Mchakato  huo  wa upatikanaji katiba mpya ambao teyali umeanza kuingia dosari kwa kitendo cha Baadhi wajumbe wanaounda Umoja wa katiba ya Wananchi UKAWA kususa vikao hivyo vya Bunge Maalum la Katiba kwa madai ya mchakato huo Kuhujumiwa na chama cha Mapinduzi CCM.
            Licha umoja huo  kususia Vikao hivyo vya Bunge Viliovyoanza leo Mkoani Dodoma bila ya kuwepo ,Lakini Bado chama cha Mapinduzi CCM,kimepuudha madai hayo ya ukawa na kuendelea na kazi ya kujadili Rasimu ya pili iliyowasilishwa na Tume ya ukusanyaji wa Maoni.
           Umoja huo wa UKAWA ni muunganiko wa Vyama vya kisiasa ikiwemo, CUF, DP na NCCR-Mageuzi vilivyosusia na kutoka nje ya Bunge,pamoja na wajumbe 201 waliochaguliwa na Rais,
              Lakini Vikao hivyo vya Bunge la katiba vimeanza leo bila ya kuwepo UKAWA,ambapo Mwenyekiti wa Bunge hilo Samweli Sitta alijinadi na kusema wananchi wategemee kupata katiba bora yenye kuwaletetea Maendeleo.
           Sitta,ambaye pia ni Waziri wa Uhusiano wa Afrika Mashariki alisema hata kama upande mmoja ya wanaojiita UKAWA kutokuwepo Bungeni haitazuia wao kutotengeneza katiba.
             Duru za mbalimbali za Kisiasa zinasema kauli hizo za Samwel Sitta zinaweza kuvuruga Amani ya nchi kutokana na yeye kushindwa kujua kwamba Katiba inatokana na Maridhiano,ambaye Waziri Sitta anapuuzia suala hilo.

No comments