Zinazobamba

URAIS NDANI CCM NI KAA LA MOTO,NAYE WAZIRI MKUU PINDA NAYE AJITOSA RASMI AANZA KUPANGA MAKUNDI YAKE SOMA HAPA UONE JINSI ALIVYOKAMIA



 
 Picha ya Waziri Mkuu Mizengo pinda,picha na Maktaba

Na Karoli Vinsent
 UWEZEKANO wa chama cha Mapinduzi kugawanyika kunakosababishwa na  wasaka Urais ndani ya chama hicho,uwezekano huo unazidi kuonekana baada ya hivi sasa  naye Waziri mkuu, Mizengo Pinda naye kujitosa Rasmi kwenye Dibwi hilo na kujihakikisha anashika nafasi ya Kumrithi Rais Jakaya kikwete,anayemaliza mda wake mwakani 2015,Mtandao huu umedokezwa.
        Waziri mkuu Mizengo Pinda,anaungana na Wasaka urais ndani ya chama hicho ambao nao wanasaka urais kufa na kupona ni Waziri mkuu aliyejiuzuru,Edward Lowassa,Waziri wa ushirikiano na Uhusiano wa Afrika Mashariki,Samwel sitta,Naibu waziri mawasiliano,Sayansi na Teknolojia,January Makamba,Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya tatu,Fredrick sumaye,pamoja Waziri wa mambo ya Nje,Berdard Membe.

        Taarifa ambazo Mwandishi wa Mtandao huu,amedokezwa Zinasema kwa Waziri Mkuu Pinda,ameanza kuanda vikao vya siri na Kuhakisha anashika nafasi ya kumrithi Rais Kikwete,ambapo Pinda anajivunia ukaribu aliokuwa nao Rais kikwete huku akijiona unaweza kumpa mwanya na sifa ya  kuweza, kuchukua Nafasi hiyo ya Urais.
       Taarifa hizo za ndani zinasema Waziri mkuu huyo teyali ameshafanya Vikao vya Siri,ambapo amefanya vikao,Jijini Dar es Salaam,pamoja na Dodoma,kabla ya kwenda Jijin London,nchini Uingereza,wiki zilizopita.
         Chanzo hicho kilizidi kusema katika kikao kimoja kilichofanyika Jijini Dar Es Salaam,kilihudhuriwa na Wanasiasa Mbalimbali ,huko akiwemo meya mmoja kutoka jiji la Dar Es Salaam ambaye jina lake tunalihifadhi,
         Katika Kikao hicho Pinda alitumia nafasi kubwa ya kuwambia wanasiasa walikuwemo kwenye kikao hicho,kwamba a lazima ndoto yake itimie kushika nafasi hiyo kubwa ya nchi,huku Waziri mkuu huyo alitumia mda mwingi akielekeza maneno kwa Wasaka Urais ndani ya chama chake kwamba hawana sifa.
        Kuibuka huko kwa Mizengo Pinda kumekuja huku ikiwa bado Kamati kuu ya chama chama Mapinduzi CCM,kikiwa kime kimewazuia wanachama wake kutotangaza nia yoyote kwenye Nafasi Urais,
          Katibu wa Itikadi wa Chama cha Mapinduzi CCM Nape Nnauya,alizidi kupigia msumari suala hilo,Alhamisi iliyopita Wakati wa Mkutano wa Waandishi wa Habari,ambapo alisema chama chake kinafuatalia kwa ukaribu mienendo ya Wanachama waliopewa Adhabu na Kamati kuu ya (CC)na kuongeza kwamba Kamati kuu itapitia upya wanachama wake sita waliopewa karipioa kwa kosa la kutangaza Nafasi mapema.
       Kuibuka huku kwa Waziri mkuu mizengo Pinda kunazidisha Homa kwa Wasaka Urais Ndani ya Chama hicho Kikongwe Barani Afrika,huku kukiwa na Sintofanu kuhusu nafasi hiyo.
         Ambapo Taarifa ambazo mwandishi mtandao huu amedokezwa zinasema Waziri wa uhusiano wa Afrika Mashariki,Samwel Sitta,jumamosi iliyopita alifanya Kampeni ya chinichini kampeni alifanya huko mkoani Kagera ambapo alipokuwa Mgeni wa Rasmi katika mahafari ya Chuo cha Wauguzi cha Mugana,kinachomilikiwa na kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba.
      Katika Mahafari hayo,Sitta alitumia mda mwingi kumtupia vijembe msaka Urais Mwenzake ambaye ni Waziri mkuu aliyejiuzuru Edward Lowassa kwa kusema hana sifa ya kuwa kiongozi katika nchi hii kutokana na vitendo vyake vya ufisadi vya nyuma.
        “Kama watajitokeza watu waongo wenye rekodi Mbaya na wasiokuwa Waadilifu,itabidi na sisi wazee tujitose katika kinyang’anyiro hicho kwani hawa wezi hawafai kushika nafasi yeyote katika nchi hii”
        “Watu hawa hukiwatazama kabisa wanaonekana ni wezi na walaghai wengine wanarekodi mbaya katika utumishi wao,yuko mwengine alihujumu mpaka nchi,eti leo anasimama kwenye majukwaa anataka urais”alisema Sitta.
        Naye Msomi wa masuala ya Kisiasa nchini kutoka chuo Kikuu cha Dodoma,Seiph Yahaya.alisema kitendo cha Waziri mkuu mizengo pinda kujitosa katika nafasi hiyo ya kuwania urais,ni ishara tosha chama cha Mapinduzi CCM,kinaweza kugawanyika.
          “Sikiliza mwandishi,tunajua kabisa Rais Jakaya Kikwete anamuandaa Mizengo pinda,ashike nafasi hiyo ya Urais,na mimi nakwambia kama Rais  leo tupangiwe na Rais Jakaya Kikwete,basi chama hiki akifiki mbali lazima kigawanyike tu utashuhudia tu mwakani”alisema Yahaya    

No comments