Zinazobamba

ABDULRAHMAN KINANA LAWAMANI, AHUSISHWA NA MIPANGO YA KUKWAMISHA UKAWA WASIONANE NA RAIS KIKWETE KUTAFUTA MWAFAKA SOMA HAPA KUJUA KWANINI,



              
 Pichani ni KATIBU mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Abdulrahman Kinana picha na Maktaba

Na Karoli Vinsent
KATIBU mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Abdulrahman Kinana Ametajwa kuwa ni mtu anayekwamisha kupatikana kwa muafaka kati ya Wajumbe wanaounda Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi UKAWA na Chama cha Mapinduzi CCM,baada ya kupanga mpango wa kuwazuia Wajumbe wa UKAWA,kutoonana na Rais Jakaya Kikwete ili kupata Suluhu,Mtandao huu umedokezwa.
            Mpango huo wa Kinana unakuja baada ya kikao cha siri kati Msajili wa Vyama vya Kisiasa nchini,Francis Mtungi na wajumbe wa UKAWA pamoja na wajumbe wa chama cha Mapinduzi kikao hicho kuvunjika na kutopatikana kwa mwafaka,

        Chama CCM,ambacho ni wapangaji katika ikulu ya Tanzania,kimeamua kupanga mpango huo wa UKAWA kutokutana na Rais Kikwete huku wakigopa kasi waliyokuwa nao,ambayo inaweza kubadilisha mwelekea wa CCM,
           Chanzo hicho kinasema Hofu ya Kinana pamoja na chama chake inatokana na Wajumbe wanounda umoja huo wa UKAWA,kuwa na nguvu na kuweza kushawishi Rais Kikwete na kuweza kuyakubali Mapendekezo hayo na kuanza kuyatekeleza,
           Mapendekezo hayo ambayo chama cha Mapinduzi CCM,wanayahofia ni Pendekezo la UKAWA kutaka Rasimu iliyowasilishwa Bungeni ambayo inaunga mkono Muundo wa Serikali tatu ijadiliwe  na kutupia Mbali Rasimu ya kipropanga ya chama cha Mapinduzi CCM,inayopigia chapuo muundo wa Serikali mbili.
Kitu ambacho kinaweza kumfanya Rais Jakaya Kikwete kukubali pendekezo hilo na kupelekea wajumbe wanaunda ukawa kurudi Bungeni,na kukiacha chama chake kikiangaika.
            Wingu,zito bado likiwa limetanda ndani ya chama cha Mapinduzi CCM,kuhusu ni hatua zipi zitumike hili kuokoa mchakato huo wa Katiba mpya ,ambao unaonekana kutoweza kupatikana kutokana,hatua iliyoko sasa ambayo baada kila upande kutopatiwa ufumbuzi huku kukiwa na jitihada za kuokoa mchakato huo zinazofanywa na msajili wa vyama vya Kisiasa nchini kugongwa mwamba.
          Hoja ya UKAWA kutaka kujadiliana na marais wawili ililenga kumpa fursa Rais Kikwete kurejesha nyuma msimamo wake kuhusu rasimu ya pili ya katiba, maana siku alipozindua Bunge la Katiba, aliweka msimamo ambao ndio umekuwa ukifuatwa na wajumbe wote wenye maslahi na CCM.
         Mara kadhaa, baadhi ya watu mashuhuri na taasisi zimesema kwamba kama Rais Kikwete asingeleta msimamo wa chama chake bungeni, ingejadiliwa rasimu ya tume, na UKAWA wasingetoka.
             Miongoni mwa watu maarufu waliokiri kwamba rais alikosea ni pamoja na Msajili ya Vyama vya Siasa mstaafu, John Tendwa, ambaye alikiri kwamba rais aliteleza.
           Jumuiya ya Wakristo Tanzania (CCT) ilitoa waraka wake kusisitiza hoja hiyo, kwamba kauli ya rais ndiyo ilivuruga mchakato, na kwamba ili Bunge liendelee kwa amani inabidi wajumbe wote wajielekeze kwenye rasimu ya pili ya katiba iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
        Mara kadhaa, viongozi wa UKAWA wametamka wazi kwamba iwapo mjadala wa Bunge hilo hautajikita katika rasimu hiyo, hawatarejea bungeni.
Serikali imekuwa inafanya jitihada za chini chini, na za wazi kuhakikisha wajumbe wa UKAWA wanarudi bungeni, lakini wao wanadai kwamba hawawezi kurudi kujadili rasimu ya CCM badala ya rasimu ya wananchi iliyowasilishwa na Jaji Warioba.

No comments