Pathfinder international wazindua huduma mpya, sasa wawasaka wagonjwa wa TB kwa simu

Mpango wa kuibua wahisiwa wa ugonjwa wa TB hapa nchini umezinduliwa rasmi mapema hivi karibuni katika wilaya ya Kinondoni, dhamira kubwa ikiwa ni mpango wa kuwatafuta waathirika wa ugonjwa wa TB katika manispaa ya hiyo ili waweze kufikisha hosptari na kupatiwa huduma
Akizungumza na mtandao huu Deputy country representatives wa PATHFNDER intenational Dr. Pasiens Mapunda amesma kuwa wameamua kuzindua mpango wa kuwasaka waathirika wa ugonjwa wa TB kokote pale walipo ili kuweza kuwasaidia kuimalisha afya zao ,
![]() |
| Hapa wananchi wakituma ujumbe mfupi . |
Wakati akizungumza na mabibi na mabwaa afya wa ngazi ya mtaa katika
wilaya ya Kinondoni, Mapunda amesema, ugonjwa wa TB bado ni tishio na kwamba
ili kunusuru maisha ya watanzania wenzetu tunaona ni vyema sasa wagonjwa watoe
ushirikiano wa kutosha kwa kutoa taarifa kwa nyia ya simu yake ya mkononi
Akizungumzia mikakati ya kuwatafuta wagonjwa hao, Mapunda amesema ili kuwafikia wananchi wengi na wao waweze kutoa taarifa zao kwa wakati wameamua kuzindua huduma hiyo kwa njia ya simu ambapo mwananchi anaweza kutuma taarifa zake kuhusiana na hali anayoiona kupitia namba 15077,
Mapunda amesema mteja anashauriwa kutuma ujumbe mfupi kwa
kuandika Neno TB kasha atume Kwenda 15077 na kasha atatumiwa maswali
anayotakiwa kujibu ili kubaini hali ya mgonjwa anayetuma taarifa hizo
Mapunda anasema, Kupitia mpango huu mpya wanategemea
wananchi wengi watajitokeza kwa wingi kutaja matatizo yao kuhusiana na ugonjwa
huu ili waweze kutambulika na kusaidia kupata huduma inayostahili kwa wakati na
bila malipo,
Aidha kuhusiana na Gharama za kutuma meseji kwa njia ya
mtandao kupitia simu yake ya mkononi, Mapunda amesema Mgonjwa hatahusika na
gharama yeyote, hivyo anawashauri wagonjwa wasisite kutoa taarifa mapema
kupitia njia hiyo mpya waliyoibuni kwa sasa,
Naye afisa mipango wa shirika la PATHFINDER intenational, Bi
Anna W.Mwakibete, ameweka bayana mbele ya mwandishi wa habari hizi kuwa shirika
la Pathfinder International limedhamilia kuwasaidia wagonjwa wa TB na hivyo
anawashauri watanzania hususani wakazi wa wilaya ya Kinondoni na Mitaa yake
kutoa taarifa juu ya ugonjwa huu kwa mgonjwa anayeonekana kuwa na dalili za TB
ili aweze kupatiwa msaada wa haraka ,
Ukiona kuwa kunamgonjwa nyumbani kwako tunaomba tutumie
taarifa kupitia simu yako ya mkononi kwa kuandika ujumbe mfupi ukianza na neon TB
kasha tuma kwenda namba 15077 kisha jibu maswali yatakuja na baada ya hapo
utafahamisha hospitari ya kwenda,
Mpaka sasa Mapunda amesema huduma hii ya kutafuta wagonjwa
wa TB kutumia simu inapatikana katika kata 13 za wilaya ya Kinondoni, ambazo ni kata
ya Goba,Kijitonyama, Makuburi,Makurumla, Mburahati,
Tandale,Hananasif,Kinondoni,Makumbusho, Mbezi-Kimara,Mwananyamara,Kawe na
mabibo.
“Tumeanza majaribio ya mpango huu hapa Kinondoni na tukiona
mafnikio basi tutakwenda Tanzania nzima, sababu sisi lengo letu ni kuona
watanzania hawasumbuliwi na ugonjwa huu wa TB” alisema Mapunda

No comments
Post a Comment