Zinazobamba

UZINDUZI WA KUFA MTU KUFANYIKA CHUO CHA TAIFA CHA USAFIRISHAJI, SOMA HAPA USIPITWE NA WAKATI...


 Ni siku ya Ijumaa tarehe 6 june,ndani ya ukumbi mkubwa wa MAKUTI HALL chuo cha usafirishaji ambapo wanavyuo kutoka sehemu mbalimbali wakichanganyika na watu wao katika kupata elimu,burudani sambamba na uzinduzi wa nguo za designer Mchox ziitwazo DUFU,akiongea na Swahili24 Blog,Masoud Mohammed ambaye ni mratibu wa onesho hilo amesema maandalizi kwa kiasi kikubwa yamekamilika na anawashukuru wadhamini wote walioweza kuongeza nguvu kwenye show hiyo akiwataja kama ifuatavyo Serengeti Breweries,Global Publishers,Swahili24 blog,Lin Collection,Epiq Media Production,Mchox Boutique,Omega Incorporation,Tayoa,Cocacola Kwanza ltd,Mwananchi Communication,National Institute of Transport,Pilipili Entartainment ltd na Burn Records. 
Masoud aliongeza kwamba,siku hiyo mida ya asubuhi kutakuwa na bonanza litakalokutanisha wanafunzi wa vyuo mbalimbali na wafanyakazi wa Global Publishers na N.I.T sambamba na  zoezi la utoaji damu kwa hiali,zoezi litakalosimamiwa na Tayoa.
Zoezi la utoaji damu litaenda sambamba na unywaji wa soda,bia na vinjwaji vingine vya kuirudisha damu iliyotolewa.Pia Masoud aliongeza kwamba kwenye bonanza hiyo kutachezwa mechi ya kugombania ngao ya hisani ambapo mshindi atapata kikombe na pesa taslimu.
Show hiyo itahamia usiku ambapo mbunifu wa mavazi Fadhil Mchongoma a.k.a Mchox atazindua mavazi yake akisindikizwa na wanamuziki na watu maarufu kibao ambao kwa uchache ni Vedasto,Country Boy,Babuu,Shadoo,Man Afro huku kwa mara ya kwanza Ayoub Alex a.k.a Sabodo anasimama mbele ya watu zaidi ya 400 akichekesha.
Upande wa watu maarufu watakao show luv kwa Red Carpet ni Monalisa,Natasha,Sheddy Clever,Tinny WHITE,JB,na wengine kibao.




Mwisho mratibu alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wadhamini wakuu wa tamasha hilo ambao ni Serengeti Breweries,Lin Collection,Swahili24 blog,Omega incorporation,mkuu wa chuo cha usafirishaji,mkurugenzi mkuu wa Pilipili Ent.,Mchox Boutique,Epiq media Production,cocacola kwanza ltd,na tayoa.





No comments