Zinazobamba

YONNA AIBOMOA CHADEMA, AHOJI UHALALI WA MUUNGANO WA UKAWA, ASEMA HABIBU ZA REJEA ZIKO WAPI?????

Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Temeke Joseph Yona Patrick akizungumza na waandihsi wa habari mapaema hii leo, Yona amesma kuwa muungano wa ukawa ni wa kinafiki na uliolenga kuwachanganya wananchi kwani maamuzi makubwa kama hayo ya kuunganisha nguvu za chama lazima yangepita katika mikutano mikuu ya vyama, sasa kuungana kwao bia kujali mikutano mikuu ya vyama vyao kuna maswali mengi ya kujiuliza,

Mwenyekiti wa chadema wilaya ya Temeke leo hii amebuka na kusema kuwa muungano wa kiujanjaujanja ulioingiwa kati ya viongozi wa Chadema, Cuf na Nccr Mageuzi utakiboboa Chama cha Chadema kwani mpaka sasa kuna baadhi ya wanachama wa chama hicho hawaridhiki na hatua ya Chadema Kuungana na Cuf ,
Yonna amesema hatua ya kutoridhishwa kwa baadhi ya wanachama wa Chadema inakuja kufuatia ukweli kuwa, viongozi wa ngazi ya juu walijaribu kuwaaminisha wanachama wa Chadema kuwa Vyma vya CUF na vingine hapa nchini ni baadhi ya mapandikizi ya Ccm hivyo kuungana nao ni sawa na kuua kasi ya mapinduzi katika nchi hii,
Amesema kama viongozi hao waliwatukana wenzao wa Cuf na vyama vingine leo hii iweje vyama hivyo vionekane vinafaa katika siku hizi za karibuni, Alihoji Bw. Yonna,Je ndoa Ya ccm N a Cuf imevunjiaka? na ni lini ndoa hiyo imevunjika?, 
amesma Chadema wamekuwa wakiwaamisha wanachama waake kuwa Mwenyekiti wa Nccr mageuzi ni pandikizi la Ccm, na ndio maana amechaguliwa na Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kuingia bungeni, Je Hivi  hiyo ndoa ya CCM na Nccr mageuzi imevunjwa lini na wapi??? alihoji Bw. Yona,

Yonna akifafanua jambo mbele ya mwandishi mwandamizi wa fullhabari blog, Yonna ameamua kufunguka Yote leo hii wakati akitoa tamko la baadhi ya wajumbe wa balaza kuu na mkutano mkuu wa Chadema kwa mikoa ya DSM, PWANI na Tanga kuhusiana kupinga uhuni wa kisiasa unaoitwa ukawa.

Akitoa Tamko lao la kupinga muungano wa kinafiki usiokuwa na habibu za rejea juu ya dhamira ya muungano wao, Yonna amesema wanachama wa CUF, CHADEMA na NCCR mageuzi sasa wamebaki njia panda kwani hawajui sasa hatima ya ukweli wa siasa ya Bongo,amesema hususani watu makini wenyekujali mustakabali wa taifa lazima wamebaki njia panda kwani,maamuzi ya kuingia katika muungano wa kinafiki umefanywa na watu wachache

Hapa Yonna akisoma Tamko la kupinga uhuni wa kisiasa unaitwa ukawa mapema hii leo, Yonna anadai kundi la ukawa ni sawa na kikundi cha sudani kusini chenye nia ya nchi kutotawalika,

Akizungumzia hatua za ukawa kususia bunge, Mwenyekiti huyo amedai kuwa hatua hiyo wanaikemea vikali kwani uwanja wa kujenga hoja ni bungeni na hatua ya kutoka ni sawa na kuogopa mambano,
Ameshauli viongozi hao kulea bungeni ili katiba mpya iandikwe na kama hawatalejea basi wao watakuwa na lakujibu kwani fursa ya kuandika katiba mpya tumeidai kwa muda mrefu lakini tulikuwa hatuipati lakini sasa tumeipata ni vyema tukaitumia ipasavyo.

Amesema wakiona hawawezi kabisa basi watangaze nafasi zao ili tufanye uchaguzi wa kuwapeleka watu watakaotetea taifa hili, kwa nguvu zao zote na sio watakaoendeshwa na misingi ya kimaslahi yao binafsi.




No comments