Zinazobamba

Al-Shabaab kuunga mkono Boko Haram kunaonyesha udhalimu wa kikundi hicho kwa watoto


Na Cleophus Tres Thomas III, Nairobi na Fuad Ahmed, Mogadishu
Wakati kikundi cha Kiislamu cha Nigeria cha Boko Haram kilipoteka nyara wasichana wa shule 276 mwezi uliopita, kilipeleka wimbi la mshtuo ulimwenguni kote na kulaumiwa katika sehemu kubwa.
Picha ya video iliyohifadhiwa katika picha za kawaida iliyochukuliwa tarehe 12 Mei, 2014, kutoka kwenye video ya kikundi cha Kiislamu cha Nigeria cha Boko Haram inaonyesha wasichana wa shule waliotekwa wakiwa wamevaa hijabu ndefu na kushikilia bendera inayohusishwa na Uislamu wa siasa kali. Boko Haram imechukua ukurasa kutoka kwenye kitabu cha michezo cha al-Shabaab, wakidai katika video hiyo kuwa wasichana hao wamebadilishwa kuwa Waislamu na kuonyesha wakirudiarudia swala. [AFP PHOTO / BOKO HARAM]

Utekaji nyara wa tarehe 14 Aprili katika mji wa Chibok wa Nigeria hata hivyo ulihamasisha lawama kali na kutoafikiwa na kikundi shirika chenzao cha al-Qaeda. Lakini tukio hilo limeungwa mkono na kikundi kimoja: kutoka kwa al-Shabaab.

Al-Shabaab, ambayo pia ina desturi ya utekaji watoto kwa kutumia nguvu na kuwaingiza jeshini kupigana, ilitoa sauti ya kuunga mkono kitendo cha kikundi cha Nigeria kupitia ukurasa wa Facebook wa Redio al-Andalus.

Katika mfulululizo wa taarifa kuanzia tarehe 10 Mei, al-Shabaab ilihoji kwamba utekaji huo umehalalishwa kama matokeo ya unyanyasaji wa serikali ya Nigeria dhidi ya Waislamu na kwamba Boko Haram "iliwaokoa" wasichana hao wadogo kutoka kwenye ukatili huo.
Maofisa wa polisi wakipitapita katika shule hiyo katika mji wa Chibok wa Nigeria ambako wasichana wa shule zaidi ya 200 walitekwa nyara na Boko Haram tarehe 21 Aprili, 2014. [AFP PHOTO / STR]



Kama majaribio ya awali ya hoja hii, al-Shabaab katika taarifa yake moja inaonyesha mfululizo wa picha ambazo ilidai ni askari polisi wa Nigeria wanaowalazimisha Waislamu majeruhi au walemavu chini wakati ofisa "Mkiristo mdogo" anaonekana kutekeleza mauaji. Taarifa hiyo pia ilionyesha kwamba Waislamu wanapaswa kohoji dhidi ya vitendo hivi na "kumwaga damu" kulipa kisasi.
CRDIT SWAHILIVILLA BLOG

No comments