Al-Shabaab kuunga mkono Boko Haram kunaonyesha udhalimu wa kikundi hicho kwa watoto
Wakati kikundi cha Kiislamu cha Nigeria cha Boko Haram kilipoteka nyara
wasichana wa shule 276 mwezi uliopita, kilipeleka wimbi la mshtuo
ulimwenguni kote na kulaumiwa katika sehemu kubwa.

Picha ya video iliyohifadhiwa katika picha
za kawaida iliyochukuliwa tarehe 12 Mei, 2014, kutoka kwenye video ya
kikundi cha Kiislamu cha Nigeria cha Boko Haram inaonyesha wasichana wa
shule waliotekwa wakiwa wamevaa hijabu ndefu na kushikilia bendera
inayohusishwa na Uislamu wa siasa kali. Boko Haram imechukua ukurasa
kutoka kwenye kitabu cha michezo cha al-Shabaab, wakidai katika video
hiyo kuwa wasichana hao wamebadilishwa kuwa Waislamu na kuonyesha
wakirudiarudia swala. [AFP PHOTO / BOKO HARAM]
Utekaji nyara wa tarehe 14 Aprili katika mji wa Chibok wa Nigeria hata
hivyo ulihamasisha lawama kali na kutoafikiwa na kikundi shirika chenzao
cha al-Qaeda. Lakini tukio hilo limeungwa mkono na kikundi kimoja:
kutoka kwa al-Shabaab.
Al-Shabaab, ambayo pia ina desturi ya utekaji watoto kwa kutumia nguvu
na kuwaingiza jeshini kupigana, ilitoa sauti ya kuunga mkono kitendo cha
kikundi cha Nigeria kupitia ukurasa wa Facebook wa Redio al-Andalus.
Katika mfulululizo wa taarifa kuanzia tarehe 10 Mei, al-Shabaab ilihoji
kwamba utekaji huo umehalalishwa kama matokeo ya unyanyasaji wa serikali
ya Nigeria dhidi ya Waislamu na kwamba Boko Haram "iliwaokoa" wasichana
hao wadogo kutoka kwenye ukatili huo.

Maofisa wa polisi wakipitapita katika
shule hiyo katika mji wa Chibok wa Nigeria ambako wasichana wa shule
zaidi ya 200 walitekwa nyara na Boko Haram tarehe 21 Aprili, 2014. [AFP
PHOTO / STR]
Kama majaribio ya awali ya hoja hii, al-Shabaab katika taarifa yake moja
inaonyesha mfululizo wa picha ambazo ilidai ni askari polisi wa Nigeria
wanaowalazimisha Waislamu majeruhi au walemavu chini wakati ofisa
"Mkiristo mdogo" anaonekana kutekeleza mauaji. Taarifa hiyo pia
ilionyesha kwamba Waislamu wanapaswa kohoji dhidi ya vitendo hivi na
"kumwaga damu" kulipa kisasi.
CRDIT SWAHILIVILLA BLOG
No comments
Post a Comment