Zinazobamba

VIJANA TUMIENI UMOJA WENU KUSHAWISHI WAJUMBE WENU WA BALAZA LA KATIBA, NI KATIKA KUYAINGIZA MAMBO MUHIMU YOTE YA VIJANA- MEYA



Na Selemani Ahamadi
Vijana wametakiwa kuhakikisha kuwa mambo yao muhimu yanajumuishwa katika katiba inayoendwa kuundwa kwa kutoa ushawishi wa vitu wanavyotaka viwemo katika katiba hiyo kwa wajumbe wao wa balaza la katiba ili mambo hayo yaweze kutetewa kwa nguvu zote katika mabalaza ya katiba



MEYA WA MANISPAA YA ILALA MH. JERRY SLAA AKIFAFANUA JAMBO KWA VIJANA WALIOHUDHURIA KONGAMANO LA KUJADILI RASIMU YA KATIBA JIJINI DARESALAAM
 Wito huo umetolewa na meya wa manispaa ya Ilala Bw. Jerry Slaa wakati akitoa mada kwa vijana wapatao 120 toka wilaya 50 za Tanzania bara na visiwani katika kongamano la vijana lililofanyika mapema hii leo jijini Daresalaam

“Haki kama ya kijana kuchaguliwa kuwa mbunge rasimu inasema ni lazima afike umri wa miaka 25 wakati umri wa jumla kwa mwananchi kuruhusiwa kupiga kura ni kuanzia miaka 18, hii inamaanisha kuwa kijana mwenye umri wa miaka 18hadi 24 hana haki ya kuchaguliwa kuwa mbunge wakati huo huo ana haki ya kuchagua mbunge wake hii sio haki hata kidogo” aliongeza Bw. Slaa

Amesema kuna watu vijana lakini wamefanya mambo makubwa kabisa na pia wapo watu wazima wameshindwa kufanya kazi nzuri kama ya kijana,hivyo kudhani kuwa kijana hawezi kufanya kazi nzuri si kweli kwani vijana wanaweza




BAADHI YA VIJANA WALIOHUDHURIA KATIKA KONGAMANO HILO WAKIMSIKILIZA KWA MAKINI MH JERRY SILAA


 Aidha katika hatua nyingine Slaa amewataka vijana naviongozi wa ngazi mbalimbali kuiangalia katiba kwa maslahi ya taifa letu na wala wasiweke maslahi ya chama ama taasisis yeyote kwani chama kinapita lakini taifa lipo vizazi na vizazi
“Hata unapoenda kuwashawishi wajumbe wenu wa balaza la katiba hakikisheni mnashawishi mambo ambayo yana masilahi kwa taifa,kwani kufanya hivyo kutasaidia kuingiza masuala muhimu ya kulijenga taifa letu “amesema Bwana Slaa
Akitolea mfano wa maeneo ambayo vijana hawana budi kuyaangalia ni pamoja na maeneo ya elimu, haki za kupiga kula ambazo kwa kiasi fulani zimeonyesha udhaifu katika rasimu ya katiba ambayo inaenda kuchambuliwa katika mabalaza ya katiba
KAIMUMKURUGENZI WA TYC NDUGU LENIN KAZOBA AKIFAFANUA JAMBO KWA WAANDISHI WA HABARI
 Naye kwa upande wake Kaimu mkurugenzi wa Taasisis ya vijana Tanzania Youth Coalition (TYC) Bw. Lenin  Kazoba ambayo ndio walioandaa kongamano hilo, amewataka vijana kushikamana pamoja ili sauti zaoili ziweze kusikika katika katiba mpya
Kongamano hilo ambalo limeandaliwa mahususi kabisa kwa lengo la kuwapa fulsa vijana kutathmini mchakato wa kutengeneza katiba, kujadili rasimu ya katiba limelenga kutoa maoni ya vijana ambayo yatawasilishwa kwenye tume ya mabadiliko ya katiba na wadau wengine wa maendeleo ili yaweze kusikilizwa na kuingizwa katika katiba mpya

MWISHO

No comments