Zinazobamba

Tanesco yaanzisha kitengo cha kushughulikiawateja wake wakubwa,CTI wasema ni wakati muafaka


Kampuni ya TANESCO imewahakikishia shirikisho la viwanda na wafanyabiashara CTI kuwapatia umeme wa uhakika na kwamba kwa kuanzia wameanzisha idara itakayoshughulika na wanachama wa shilikisho hilo moja kwa moja kutatua kero zao zinazowakabili

Akizungumza katika mkutano maalum uliowashirikisha wanachama wa shirikisho hilo la CTI na uongozi wa kampuni ya Tanesco mapema hii leo, Mkurugenzi mtendaji wa Tanesco Eng Felchesmi Mramba amesema hatua ya kuwa na kitengo cha huduma kwa wateja wanaotumia kwa kiasi kikubwa umeme wa Tanesco umefikiwa ili kuweza kuwa karibu na watumiaji hao na wao pia kuweza kutoa kero zao kwa muda muafaka na kupatiwa ufumbuzi wa haraka

KAIMU MKURUGENZI MTENDAJI WA TANESCO eNG. FELCHESMI MRAMBA AKIFAFANUA JAMBO KUHUSU UHAKIKA WA UMEME KATIKA JIJI LA DARESALAAM


Eng Mramba ameendelea kusema kuwa kwa sasa wamiliki wa viwanda, na wafanyabiashara wakubwa wamekuwa wakitumia takribani asilimia 60 ya umeme wote unaodhalishwa na Tanesco hivyo ili kuweza kuwajali na kusikia kero zao kwa karibu tumeamua kuweka kitengo hicho ambacho tunaamini kitasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza kero ambazo walikuwa wanakumbana nazo

“Tunaamini kwa ushirikiano tutakaouonyesha utaweza kuwawezesha wamiliki wa viwanda na wafanyabiashara wakubwa kuongeza uzalishaji wao kwa kiasi kikubwa na hivyo kuweza kuinua uchumi wa taifa letu” aliongeza Eng Mramab


Eng. MRAMBA AKIFUATILIA MOJA YA MAWASILISHO YA MIRADI MBALIMBALI INAFANYIWA KAZI NA KAMPUNI YAKE,WADAU WA CTI WALIPATA FULSA YA KUSIKILIZA MIRADI HIYO NA KUTEMBELEA BAADHI YA JIJI LA DARESALAAM

Aidha katika hatua nyingine Eng Mramba amebainisha miradi mbalimbali ambayo inatekelezwa na ile ambayo bado haijaanza rasmi kutekelezwa hiyo ikiwa ni jitihada za kuwahakikishia wanachama hao wa CTI kuona ni jinsi gain Kampuni imejipanga kuwepo kwa umeme wa kuaminika hapa nchini na kuwapa wanachama hao fulsa ya kujipanga namna gain wanaweza kuongeza uzarishaji wa bidhaa zao,

Miongoni mwa miradi iliyowasilishwa kwa wamiliki hao wa viwanda ni pamoja na ile miradi ya kujenga vituo vyenye megawati kubwa ya pale Ubungo,Kurasini Gongo la mboto na Kinyerezi ambapo ikimalizika hakutakuwa na tatizo la umeme kabisa katika jiji la Daresalaam


MWENYEKITI WA SHIRIKISHO LA VIWANDA NA BIASHARA CTI AKIFAFANUA JAMBO KWA WANACHAMA WA CHAMA HICHO MAPEMA HII LEO KATIKA OFISI ZA TANESCO
                                

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa shirikisho la viwanda na wafanyabiashara CTI BW. Felex Mosha amepongeza hatua zilizochukuliwa na uongozi wa Tanesco kwa kuandaa idara itakayoshughulika moja kwa moja na wanachama wake kwani hatua hiyo inategemewa kuongeza tija kwa wafanyabishara na wamiliki wa viwanda kwa kupatiwa umeme wa uhakika

MMOJA WA WANACHAMA WA CTI AKIFAFANUA JAMBO MBELE YA MKURUGENZI WA TANESCO MAPEMA HII LEO
                                

Aidha Bw. Mosha amepongezajuhudi za kuwaleta pamoja wadau wa umeme na kukaa meza moja kuzungumzia pamoja kero za umeme katika viwanda vyetu na kwamba  kuanzia sasa sisi kama wamiliki wa viwanda tutakuwa katika nafasi nzuri ya kujua kinachoendelea katika suala zima la umeme na kuwataka viongozi hao wasiishie kuwaita tu katika mikutano na badala yake watoe taarifa za umeme kwa haraka zaidi ili waweze kuchukua tahadhari mapema
“Tunawomba nyinyi kama tanesco kutupatia taarifa ya katizo la umeme mapema iwezekanavyo ili tuweze k

MDAU AKIMAKINIKA KUFUATILIA MADA ZINAZOENDELEA

HAPA WADAU WA CTI WAKIONYESHA MOJA YA VITUO VYA KISASA CHA UBUNGO AMBACHO KITASAIDIA KUPUNGUZA TATIZO LA UMEME HAPA JIJINI, KINADHALISHA JUMLA YA KW 180

     
CTI  WAKIWA WANAANGALIA MITAMBO YA KUZALISHA UMEME WA UHAKIKA








ujiandaa, na tunaamini kwa sababu ninyi ni sura mpya basi hata matendo yenu yatakuwa mapya na ndio maana hata leo tumeanza ushirikiano mpya na nynyi” aliongeza Bw Mosha
Wamiliki hao pia wamepata fulsa ya kujionea miradi mbalimbali inayoendelea katika jiji la Daresalaam

No comments