Zinazobamba

TAPELI MAALUFU LAKAMATWA DAR,


Na Selemani magari
JESHI la polisi kanda maalum ya jiji la Daresalaam, limefanikiwa kumkamata Mfaume Omari Maalufu kwa jina la Mau mkazi wa magomeni kagera kwa tuhuma za utapeli  ambaye alikuwa akitumia majina ya watu maarufu,viongozi wa serikali  na viongozi wa dini vibaya ili kujinufaisha yeyemwenyewe
 
Bw. Mau alikuwa akifanya utapeli huo kwa kujivisha uhusika wawatu maarufu na kuanza kuomba fedha kwa watu mbalimbali kupitia namba za simu ambazo amekuwa akizitoa kwa njia ya facebook,ambapo watu wengi wamekuwa wakiamini kuwa yeye ni kweli muhusika wa cheo alichojivisha na ndipo watu hao walipoanza kumtumia pesa kupitia namba za simu ambazo amezichapisha katika mtandao wa facebook

KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI KANDA MAALUM YA DARESALAAM DCP ALLY MLEGE  (KUSHOTO) AKIFAFANUA JAMBO MBELE YA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU KUKAMATWA KWA TAPELI MAARUFU HAPA JIJINI
Akizungumza na Wandishi wa habari ofisini kwake Kaimu Kamishina wa polisi kanda maalum ya Daresalaam Bw. Ally Mlege amesema kukamatwa kwa tapeli huyo hatali kumekuja kufuatia taarifa iliyotolewa na Mh.(Mb) na mchungaji Getrude Rwakatare na kulifikia jeshi la polisi kuwa jina lake linatumiwa vibaya na mtu anayemtakia mabaya kupitia njia ya mtandao na ndipo uchunguzi ulipoanza na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo namba moja wa utapeli kwa kutumia mitandao

Kamishina Mlege ameendelea kusema kuwa baada ya kukamatwa mtuhumiwa huyo amekutwa na simu kadi mbili moja ikiwa imesajiriwa kwa jina la Mfaume Saidi Omari yenye namba 0659736454 na nyingine ikiwa imesajiriwa kwa jina la Alex Mtenga yenye namba 0659164744 ambazo zote alikuwa akizitumia kuombea pesa kwa watu maalufu kwa njia ya mtandao

Kamishina Mlege ameongeza kusema kuwa mtuhumiwa huyo wa utapeli amekiri kuhusika na utapeli wa njia ya mtandao kwa watu ambalimbali wakiwemo wachezaji maarufu wa timu za mipira hapa nchini  kwa kuvaa uhusika wa wa watu maarufu waliostaafu, mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi la polisi na atafikisha mahakamani ushahidi utakapokamilika

No comments