TUMEZITAMBUA RASMI BLOGS, SASA ANDIKENI MAZURI NA SI KUCHAFUANA, NKOMA
| MKURUGENZI WA TCRA PROF. JOHN NKOMA AKIFAFANUA JAMBO MBELE YA MKUTANO WA WADAU WA MAWASILIANO, |
TCRA SASA YAANZA KUZITAMBUA BLOGS, WADAU WASEMA NI HATUA
NZURI KWA SERIKALI KUZITAMBUA
Kufuatia ukuaji wa
watumiaji wa mitandao kuongezeka kila kukicha huku wamili wa mitandao ya
kijamii wakiendelea kuongezeka kila leo, malaka ya mawasiliano Tanzania Imeamua kuwatambua rasmi
wamiliki wa mitandao hiyo ya kijamii kuwa ni moja ya vyombo vya kuaminika kwa
kutoa taarifa za kuelimisha, kuburudisha na kuonya wananchi
Akizungumza katika kampeni maarum ya kuhamasisha matumizi
mazuri ya mawasiliano kwa wananchi, mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya mawsilano
TCRA Bw. Amesema wameamua kuwatambua rasmi mitandao ya kijamii kama inamchango mkubwa sana wa kuujulisha umma habari mbalimbali
zinazoendelea ndani na nje ya nchi
Mkurugenzi huyo ameendelea kusema kuwa kwa sasa kuna idadi
kubwa ya watumiaji wa mitandao ambapo mpaka sasa jumla ya wananchi wapatao
milioni 7.6 wanaendelea kupata taarifa kupitia njia ya mitandao ukilinganisha
na idadi ya wananchi laki tatu ambao walikuwa wakitembelea mitandao kwa kipindi
cha miaka mitau iliyopita
Mkurugenzi
wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA Bw. Profesa John Nkoma
akimsikiliza Msanii Mrisho Mpoto wakati alipokuwa akitoa ujumbe wake kwa
waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha
matuzimizi mazuri ya mitandao ya mawasiliano uliofanyika katika makao
makuu ya mamlaka hiyo Sinza barabara ya Sam Nujoma jijini Dar es salaam
leo.
Hata hivyo mkurugenzi huyo
amewataka wadau wa Blogs hapa nchini kuacha tabia ya kuandika mambo ambayo
yanasababisha uvunjifu wa amani au udhalilishaji kupitia BLOGS hizo kwani
kufanya hivyo ni kinyume cha sheria ya mawasiliano ya kielectroni na posta
(EPOCA) mwaka 2010
“watanzania walio wengi sasa
wanafaidika na huduma za mawasiliano kupitia blog zenu hivyo ni vema mkaandika
vitu vya ukweli kwani ukweli utawafanya wateja wenu wakubwa wanaotembelea blog
zetu kupata vitu ambavyo si vya kubabaisha na hivyo kuweza kujijengea heshima
kwa wananchi unaowahudumia ” aliongeza Bw…
Naye mmoja wa wamiliki wa Blogs
maarufu hapa nchini Bw. Othmani Michuzi ameisifu serikali kwa hatua waliochukua
ya kuitambua rasmi mchango wa wanablog hapa nchini na kuahidi kuwa
watahakikisha wanafuata maadili yote ya uandishi wa habari ili kuweza kuwapa
wananchi vitu vya uhakika na kwa wakati
Kwa sasav Blogs zinatoa Taarifa
kwa haraka zaidi ukilinganisha na midia zingine nah ii ni kutokana na ukweli
kuwa waendesha BLOGS wote wanahakikisha taarifa zao zinawafikia wateja wao kwa
wakati
| MMOJA WA WAMILIKI W A BLOG BW. OTHMANI MICHUZI AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI |
Mkurugenzi
wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA Bw. Profesa John Nkoma
akimsikiliza Msanii Mrisho Mpoto wakati alipokuwa akitoa ujumbe wake kwa
waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha
matuzimizi mazuri ya mitandao ya mawasiliano uliofanyika katika makao
makuu ya mamlaka hiyo Sinza barabara ya Sam Nujoma jijini Dar es salaam
leo. Katika uzinduzi huo TCRA imesema kwa sasa inatambua rasmi mitandao
ya kijamii kama blogs kwamba ni vyombo kamili vya habari na kwamba kwa
sasa mamlaka hiyo inaadaa utaratibu wa kukutana na bloggers na
kuzungumza nao juu ya matumizi mzuri ya mitandao na kutafuta wataalamu
kwa ajili ya kutoa mafunzo mbalimbali juu ya matumizi ya mitandao na
ujuzi zaidi katika mawasiliano ya mitandao.
Mkurugenzi
wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA Bw. Profesa John Nkoma
akizungumza katika uzinduzi huo kushoto ni Inocent Mungi Meneja
Mawasiliano wa TCRA.
Waandishi wa habari wakiwa katika uzinduzi huo leo
Waandishi wa habari wakiwa katika uzinduzi huo leo
Elisha Elia Mwandishi wa habari wa TBC akiandika mambo muhimu yaliyoelezwa katika mkutano huo kulia ni Daula Abdul wa TBC.
No comments
Post a Comment