TANZANIA KUUZA UMEME NJE MWAKA 2014
Tanzania sasa itakuwa na uwezo wa kuuza umeme wake nje ya nchi
ifikapo mwaka 2014 baada ya TANESCO
kutiliana saini mkataba na kampuni ya
china ya kuzalisha umeme wa gesi ya mtwara.
Akizungumza katika sherehe ya kutiliana saini ya mkataba huo
waziri wa nishati na madini Sospeter Muhongo alisema kuwa kituo hicho cha
uzalishaji umeme wa gesi kitajengwa katika eneo la kinyerezi jijini Dar es
salaam na inatarajiwa kumalizika mwaka 2014
Waziri Muhongo aliongeza kuwa mradi huo utaweza kuzalisha
megawati 600 na unatarajiwa kugharimu
kiasi cha dola milioni 300 za kimarekeni
“Mradi huu ukikamilika utasaidia kuboresha uchumi wa nchi
kuongeza pato la taifa , tutaboresha barabara,shule na hospital hapa nchini”
aliongeza Waziri.
| BALOZI WA CHINA HAPA NCHINI LUI ZOGHUO AKIZUNGUMZA KATIKA SHUGHULI HIYO |
| WAZIRI WA NISHATI NA MADINI MH.SOSPETER MUHONGO,MKURUGENZI WA TANESCO MH.FELCHEMI MRAMBA WAKIMSIKILIZA KWA MAKINI BALOZI WA CHINA HAPA NCHINI |
| WAZIRI WA NISHATI NA MADINI SOSPETER MUHONGO AKIZUNGUMZA KATIKA SHUGHULI HIYO |
No comments
Post a Comment