Zinazobamba

NBC YAZINDUA KAMPENI YA MIKOPO KWA WAFANYA KAZI WAAJIRIWA




Benki ya taifa ya Biashara NBC Imezindua kampeni ya uelewa ya mikopo kwa makundi, ambapo kupitia kampeni hiyo mteja anayehitaji kukopa benki hiyo ni  lazima awe muajiriwa na kwamba sharti pekee la kukubalka ni uthibisho wa barua ya muajiri wako na sio vinginevyo

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo makao makuu ya benki hiyo jijini Daresalaam Mkurugenzi mtendaji wa benki hiyo Bi.Mizinga Melu amesema uzinduzi huo umekuja wakati muafaka kwa waajiiriwa ambao walikuwa hawapati fulsa za kuomba mikopo kwa kukosa sifa zinginezo katika benki hiyo sasa wanaweza kuomba mikopo kupia sifa za kuajiriwa,

Benki ya biashara ya Taifa inauzoefu wa kufanya huduma za kipesa hapa nchini kwa takribani miaka 45 na kwamba ina matawi zaidi ya 52 na ATM ZA VISA zisizopungua 280 nchini kote hivyo ni vema watumishi wakachangamkia mikopo hiyo

No comments