Zinazobamba

KUANZA KWA MSMU MPYA WA UNUZI WA NAFAKA,WAKULIMA WATAKIWA KUUZA MAZO YENYE UBORA WA HALI YA JUUU


Na selemani Magari

WAKALA wa hifadhi ya chakula (National food ResevesAgency) imeanza mchakato wa kununua nafaka kwa wananchi na kuwatangazia wakulima wa kanda saba za Kipawa,Arusha,Shinyanga,Dodoma,Makambako,songea na Songea kupeleka bidhaa zake sokoni zikiwa na ubora unaotakiwa
MSEMAJI WA WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA bWANA RICHADI KASUGA AKIFAFANUA JAMBO MBELE YA WANAHABARI


CHARLES WALWA, MKURUGENZI WAKALA WA TAIFA WA HIFADHI YA CHAKULA Bw. Charles Walwa akifafanua moja ya mswali ya wadau


Akizungumza na wanahabari hivi karibuni, Mkurugenzi wa wakala wa taifa wa hifadhi ya chakula Bw. Charles Walwa amesema kuwa kwa sasa tathimini fupi iliyofanywa na wizara inaonyesha kuwa hali ya chakula kwa mikoa yote 25 ni nzuri na kwamba wao wataanza mchakato wa kununua nafaka katika maeneo ambayo kuna dhiada

Ameendelea kusema kuwa katika mwaka huu jumla ya vituo 58 vitatumka katika ununuzi wa nafaka, hivyo wananchi wanashauriwa kupeleka nafaka zao katika vituo hivyo,pia ametoa angalizo kwa wananchi kupeleka nafaka kwa wakala ambazo tu zimekidhi vigezo
 
Naye mkurugenzi msaidi wa utafiti wa mazao Bw. Hussein A.Mansoor ameongeza kusema kuwa kwa sasa kumebainika ugonjwa hatari wa mahindi uitwao maize lethal necrotic (MLND) ambao umeanzia huko nchi za jirani za Kenya na kwamba tayari serikali imeshachukua tahadhari zote za kuondoa ugonjwa huo kuingia nchini,amesema ugonjwa huo kwwa sasa hauna tiba

No comments