Dr.Philip Mpango mgeni rasmi tuzo ya Mwalimu Nyerere ya uandishi bunifu.
Pia mshindi wa pili atazawadiwa kitita cha Tsh. milioni 7,huku mshindi wa tatu ataondoka na Tsh. milioni 5 na washindi wanne hadi wa 10 watapata cheti pekee.
Prof.Mkenda amebainisha kwamba maandalizi yote yamekamilika kwa asilimia kubwa na kinachosubiriwa na siku hiyo ya tukio kubwa kufika.
Aprili 13 kila mwaka ndio siku ya kumbukizi ya kuzaliwa, Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere na ndio imepangwa kufanyika kwa tuzo hiyo na huu ni msimu wa tatu.
"Mgeni rasmi kuwa ni makamu wa Rais inadhihirisha namna Serikali inavyotambua na kuweka uzito katika tuzo hiyo ya Uandishi Bunifu ambayo kwa njia moja ama nyingine inasaidia kukuza lugha ya Kiswahili kutokana na Waandishi shindani kutumia lugha hiyo katika kazi zao" amesema.
Profesa Mkenda amesema kuwa Tuzo ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu ni miongoni mwa njia bora za kuenzi fikra,falsafa na maono ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ambaye aliweka msingi wa matumizi na ukuzaji wa lugha ya Kiswahili kama nyenzo ya elimu, umoja na maendeleo ya jamii ya Watanzania.
“Tuzo hii ni heshima kwa Mwalimu Nyerere lakini pia ni jukwaa mahsusi kwa waandishi chipukizi na wakongwe kuonesha umahiri wao katika nyanja mbalimbali za uandishi kama vile riwaya, ushairi, hadithi za watoto na tamthiliya,” amesema.
Pia amesema mshindi wa kwanza licha ya kushinda Tsh.milioni 10, kazi yake itachapishwa na kutumika katika shule na maktaba nchini kwa ushirikiano na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET).
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo hiyo Profesa Penina Mlama amesema kwamba majaji wamekamilisha kazi ya kusoma na kuchambua miswaada iliyowasilishwa na tayari orodha teule ya waandishi waliopendekezwa imechapishwa.
Profesa Mlimani ameongeza kuwa hadi sasa tayari zimechapishwa kazi mbili za washindi na kazi ya tatu ipo katika hatua za mwisho kukamilika.
Post Comment
Hakuna maoni
Chapisha Maoni