Zinazobamba

RAIS MWINYI: UMOJA WA ULAYA UNA MCHANGO MKUBWA ZNZ


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi amefahamisha kuwa Umoja wa Ulaya una Mchango Mkubwa na Muhimu kwa Maendeleo na Sekta ya Uwekezaji  pamoja na ustawi wa maisha ya Wananchi. 

Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo alipofungua Kongamano la Biashara la Zanzibar na  Umoja wa Ulaya , Hoteli ya Golden Tulip, Uwanja wa Ndege ,Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi. 

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi ameuhakikishia Umoja wa Ulaya kuwa Serikali inachukua Juhudi maalum Kuandaa Mazingira mazuri ya Uwekezaji hapa nchini ili Wawekezaji wanaokuja wawekeze katika Mazingira Bora na endelevu.Halikadhalika, Rais Dkt. Mwinyi amesema Zanzibar itaendelea kushirikiana na Umoja wa Ulaya katika nyanja mbalimbali za Maendeleo kwani ni mshirika Muhimu katika  Juhudi za kukuza Uchumi.

Amebainisha kuwa Uwekezaji wa  Umoja wa Ulaya hapa Zanzibar unachangia Asilimia 31 ya  Miradi yote ya Uwekezaji iliosajiliwa  unaofikia thamani ya Euro Bilioni 2.8 na kutoa fursa za Ajira Elfu 19.

Rais Dkt.Mwinyi  alishuhudia Utiaji Saini wa Mkataba wa Ushirikiano Baina ya Umoja wa Ulaya na Mamlaka ya Uwekezaji ya Zanzibar (ZIPA) pamoja na kuzindua Ripoti ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya hapa Zanzibar ya Mwaka 2023.



Hakuna maoni