Zinazobamba

JESHI LA POLISI KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI KUANZA OPARESHENI YA KUKAMATA MAGARI NA PIKIPIKI ZENYE VINGO"ORA KINYUME CHA SHERIA

DCP Ramadhani Ng'anzi akizungumza na Waandishi wa habari katika Makao Makuu ya Kikosi hicho Jijini Dar es salaam(Na Mpiga Picha Wetu).

Na Mussa Augustine

Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini  limesema litaanza Oparesheni kabambe ya kukamata Magari yote ambayo si ya dharula yliyofungwa  vingora,Vimulimuli,Namba za Bandia,na taa za Kuongezwa kwenye vyombo hivyo vya moto  bila kuzingatia utaratibu wa kisheria.

Kauli hiyo imetolewa leo Februari 23,2024 Jijini Dar es Salaam na Kamanda wa Jeshi la Polisi Kikosi Cha Usalama Barabarani  Tanzania DCP Ramadhani Nga’nzi Wakati akizungumza na waandishi wa habari nakusema  kuwa Kuna baadhi ya watu wamejenga utamaduni wa kujihalalishia kuwa ni Sheria kuweka namba za bandia kwenye magari Yao.

Amewataka wamiliki na madereva wanaofunga vingora, vimulimuli namba za bandia na taa za kuongezwa kwenye magari na pikipiki kama Kuna ulazima wa kufanya hivyo basi wanatakiwa kuomba na kupata ridhaa ya kufanya hivyo kutoka Kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ambaye ndie mwenye dhamana ya kuidhinisha vibali hivyo.

“Wapo watu binafsi makampuni au taasisi zinafunga vingora katika magari yao na kubitumia bila kuzingatia utaratibu wa kisheria, Kwa kufanya hivyo wanaovunja  sheria ya usalama barabarani na wanastahili adhabu ikiwemo ya kulipia faini ya tozo za makosa ya usalama Barabarani au kuweka mahabusu na kuandaliwa mashtaka na kupelekwa mahakamani au vyote Kwa pamoja” Amesema DCP Nga’nzi 

Aidha DCP Nga’nzi amefafanua kuwa wananchi wanapaswa kujua kuwa taa zilizowekwa kutoka kiwandani zinaruhusiwa kisheria akitolea mfano Magari ya Mgodini na kuwindia porini nakwamba  matumizi yake yawe sehemu husika.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na DCP Ng'anzi inasema kuwa Sheria ya Usalama Barabarani sura ya 168 kama ilivyopitiwa mwaka 2002 kifungu Cha 54 (2) (5) kingora kitafungwa kwenye gari au pikipiki za dharura, mfano magari na pikipiki zitumikazo katika misafara ya viongozi, pikipiki za polisi, Zimamoto, hospitali na pikipiki za Jeshi tena kwa kuzingatia maelekezo ya Waziri mwenye dhamana ya Usalama Barabarani
   Gari likiwa limefungwa vimulimuli (Picha kwa hisani ya Mtandao)


Hakuna maoni