DUKA LA VIATU AINA YA RELAXO LAFUNGULIWA DAR ES SALAAM ,MEYA KUMBILAMOTO AMPONGEZA MWEKEZAJI
Na Mussa Augustine.
Serikali imewahakikishia kuboresha zaidi mazingira ya usalama kwa Wawekezaji na kuendelea kuwapa ushirikiano ili kusaidia Serikali kutoa ajira za kudumu na za muda mfupi kwa wazawa .
Hata hivyo Meya huyo amesema kuendelea kuwepo kwa wawekezaji hao nchini ni ishara tosha kuwa usalama upo na umeimarishwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam SACAP Jumanne Murilo katika kuhakikisha anasimamia usalama kwa Wawekezaji nchini
Kwa upande wake
Mkurugenzi wa Kampuni hiyo ya Best
brands Distributors ,Bw. Khalid Mohammed Salim amesema Kampuni yake imejipanga
kuwafikia wateja wake kwa maeneo ya karibu na Jiji ambapo Tawi jipya la Relaxo lililopo
mtaa wa Samora Posta Jijini Dar es salaam
litakwenda kuzalisha ajira kwa vijana
zaidi ya 50 kwa jiji la Dar es salaam ikiwa ni dhamira yao ya dhati ifikapo
2025 .
“Kipekee tumepata
maombi mengi ukizingatia viatu vyetu tumelenga zaidi upande wa kimichezo hivyo
wanamichezo wengi wanapenda kupata viatu vyenye ubora zaidi ndio maana tukawiwa
kuendelea kufungua matawi katikati ya mji hili la leo tumezindua ni duka la
tatu na tuna mpango wa kufungua maduka 20 sanjari na ujenzi wa Kiwanda
cha uzalishaji wa viatu hivyo ili kuwafikia wateja wetu kwa haraka kutokana na
ubora wa viatu vyetu."amesema Salim
Pia amesema Kampuni
hiyo imetoa ofa ya kuhakikisha watakaohitaji kuuza bidhaa hizo watagharamiwa
fremu za biashara ili kuendelea kuzitangaza bidhaa hizo.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni