TAMASHA LA KWANZA LA "UTULIVU EXPERIENCE" KUZINDULIWA APRIL 20 MWAKA HUU,WANANCHI WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI
Akizungumza na Waandishi wa habari leo Januari 30,2024 Jijini Dar es Salaam Mtendaji Mkuu wa Taasisi hiyo Ibrahim Rwegerera amesema kuwa uzinduzi wa Tamasha hilo utafanyika April 20 mwaka huu Bara Katika Ukumbi wa Super Dome Masaki Jijini humo,lakini pia Tamasha hlio litafanyika Mwezi Novemba 20204 Visiwani Zanzibar.
Rwegerera ameongeza kuwa Tamasha hilo litawahusisha watu wa kada mbalimbali ikiwemo watu maarufu, viongozi na wenye matokeo chanya Ndani ya Jamii.
Aidha amesema kuwa wageni waalikwa katika tamasha hilo watapata fursa ya kubadilishana mawazo na viongozi mbalimbali ikiwemo wastaafu na wale waliosaidia katika kudumisha amani na mshikamano wa Taifa.
Amesema anaamini kuwa kupitia Tamasha hilo Tanzania itasherehekea faida za amani na Utulivu ambayo Moja ya alama inayolitambulisha taifa la Tanzania Duniani kote.
“Utulivu Experience ni jukwaa ambalo limetengenezwa kwa Neema za Mungu kufurahia amani na Utulivu wa Tanzania toka enzi za Wazee wetu ambao tunategemea kupata uzoefu wa njia walizotumia kudumisha amani ambayo mpaka leo tunayo” Amesema Rwegerera.
ReplyForward |
Hakuna maoni
Chapisha Maoni