Zinazobamba

WATETEZI WA MAMA KUADHIMISHA SIKU YA KUZALIWA DR SAMIA KWA KUYASAIDIA MAKUNDI YENYE UHITAJI.

Na Mussa Augustine.

 Taasisi ya Watetezi wa Mama ambayo inajihusisha na Masuala ya Kijamii,Siasa na Kiuchumi inatarajia kufanya shughuli mbalimbali za kijamii  katika kuelekea maadhimisho ya siku ya kuzaliwa Rais Dkt Ras Samia Suluhu Hassan itakayofanyika Januari 27 ,2024.

Hayo yamebainishwa Desemba 20,2023 na Msemaji wa Taasisi hiyo Mkoa wa Dar es salaam  Madebe Lidai wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari kuelezea  namna Taasisi hiyo itakavyoshiriki ipasavyo katika maadhimisho ya siku ya kuzaliwa Dr. Samia Suluhu Hassan ambapo kauli mbiu inasema " Mama ni Fahari sote tunajivunia".

 "Januari 27 mwaka ujao ni siku ya kuzaliwa kwa Chifu Hangaya( Rais Dr.Samia Suluhu) tunatarajia kufanya shughuli mbalimbali kuelekea siku hii ikiwemo kutembelea vituo vya watoto yatima,vituo vya watu wenye ulemavu,Wajawazito wasio na misaada hospitalini,pamoja na Wajane ili kuweza kuyashika mkono makundu haya muhimu katika jamii" amesema Lidai ambaye ni maarufu kwama Nabii Mswahili.

 Sambamba na hilo Taasisi hiyo inatarajia kufanya ziara ya kutembelea Miradi inayotekelezwa na serikali ya Dr Samia Suluhu Hassani kwenye halmashauri za Manispaa zilizopo Mkoani Dar es salaam ili kuweza kuandaa Makala( Documentary) itakayo onyeshwa siku ya kuzaliwa Dr.Samia Suluhu Hassan Januari 27 ,2024.

 Awali Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Mohamed Cassim Chande amesema kwamba Rais.Dkt Samia Suluhu Hassan amedumisha Amani na Mshikamano kwa Watanzania hivyo Watanzania wanapaswa kumuunga Mkono katika jitihada zake za kulinda tunu za Taifa.

 "Sisi tuna deal( shughulika) na wale wanaobeza yale Mambo Mazuri yanayofanywa na Rais Dkt Samia,hivyo napenda kutumia fursa hii kuwaomba wale wote wanaofanya hivyo waache mara moja na 'Ukimvaa tutakuvaa kwa hoja' amesema Chande kwa bashasha.

 Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Taasisi hiyo ya Watetezi wa Mama William Frank Chitande amesema kwamba taasisi hiyo itaendelea kumuombea na Kumsemea Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri  anazozifanya za kuwaletea Wananchi Maendeleo.

 Hata hivyo  afisa Miradi wa Taasisi ya Watetezi wa Mama, Muhamad Sekamba amesema kwamba siku ya kilele cha Maadhimisho ya siku ya Kuzaliwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Michezo mbalimbali itafanyika ikiwemo Jogging ,pamoja na bonanza la Mpira kati ya Wasanii wa Bongo Movie na Waigizaji wa filamu ikiwa lengo ni kumuenzi Rais Dkt. Samia kwa Mchango wake katika kukuza sekta ya Michezo nchini.

Hakuna maoni