Zinazobamba

FCS YAFANYIA TATHMINI MRADI WA URAIA WETU UNAOTEKELEZWA NA MTWANGONET.

 Mkurugenzi wa MTWANGONET Fidea Ruanda

Na Mussa Augustine. 

Imeelezwa kuwa moja ya changamoto inazoikumba umoja wa Asasi za kiraia Mkoani Mtwara ( MTWANGONET) ni ukosefu wa elimu ya uandaaji wa tariifa ya fedha za miradi zinazotolewa na wafadhili hali inayopelekea kushindwa kuaminika kupewa tena fedha za miradi.

 Kauli hiyo imetolewa tarehe 18,2023 mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na  Mkurugenzi wa MTWANGONET Fidea Ruanda, wakati alipokua katika Semina ya kutoa tathmini ya utekelezaji wa mradi wa Uraia Wetu ambao unatekelezwa na wadau wa Asasi ya  Foundation For Civil Society (FCS) chini ya ufadhili wa Umoja wa Ulaya.

Fidea amesema kuwa, lengo la mradi huo ni kuangalia mazingira wezeshi katika kutekeleza majukumu yake na kushirikiana na Serikali ambapo wanatekeleza mradi huo katika mikoa saba ikiwemo Songwe, Ruvuma, Iringa, Njombe, Mbeya, Mtwara, Rukwa, ambapo wanasimamia Kanda ya kusini katika mradi huo huku ukilenga kwa vijana, wanawake, na walemavu ambapo unatekelzwa kwa miaka 3 kuanzia 2023 hadi 2025.

 "Uwelewa mdogo kuhusu sera, sheria na miongozo mbalimbali ikiwemo kulipa asa kwa mashirika machanga bado ni changamoto licha ya kuwa malipo ni shill 50,000 kwa mwaka kwani usipolipa hadi kufikia mwezi wa April mwaka unaofuata unapigwa faini asilimia 100 ambapo ni sawa na shill laki 100,000" amesema Fidea.

 "Tunatakiwa tuwe na umoja wetu tuongee kauli moja ,tuwe na agenda moja ya mradi wetu ili kuangalia namna ya kuuendesha mradi kwani lengo ni kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha maisha ya wananchi" amesema Fidea

Mratibu wa Miradi kutoka FCS Nicholas Lekule 

 Kwa upande wake, Mratibu wa Miradi kutoka FCS Nicholas Lekule amesema kuwa, FCS imetoa ruzuku kwa wadau kumi na tano ambao wanafanya kazi katika maeneo tofauti tofauti ikiwemo kwenye kanda, kitaifa na zile asasi zinazofanya kazi na wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, huku wadau 12 wakipokea shill mill 110, na wadau 3 wa kitaifa wakipokea shill mill 145.

 Aidha, amesema kuwa tathmini ya mradi wa Uraia Wetu iliyofanyika leo  nikutaka kuangalia lengo lake ikiwa ni kuwajengea uwezo katika asasi za kiraia ziweze kufanya shughuli ambazo zitasaidia kuleta mabadiliko ya kisera.

 "Moja ya kazi tunazofanya nikuziboresha asasi za kiraia ili ziweze kufanya kazi zenyewe ili kukabiliana na changamoto zinazojitokeza,leo watatuonyesha wao ni akina nani wamekutana na akina nani katika kutekeleza mradi huo,nichangamoto zipi na nikwanamna gani wanashirikiana na serikali na watunga sera katika kufanya kazi" amesema Nicholas



Hakuna maoni