Na
Mussa Augustine.
Waziri
wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Wanawake na Wenye Mahitaji Maalum Dkt Dorothy Gwajima amewataka
wamiliki wa Vituo vya kulelea watoto wadogo Mchana (Day care )
kuzingatia Maadili na Desturi za kitanzania nakwamba watakaobainika wanafanya kinyume agizo hilo watachukuliwa hatua za
kisheria ikiwemo kufungiwa vituo vyao.
Pia
Waziri huyo amewataka wamiliki wa vituo vya watoto wadogo Mchana na shule za
awali kujisajili ili waweze kupewa miongozo ya kuendesha vituo hivyo kwa mujibu
wa sheria.
Dkt
Gwajima ametoa kauli hiyo Jijini Dar es salaam Desemba 13,2023 wakati akifungua Mkutano wa Umoja wa
wamiliki wa vituo vya Kulelea Watoto Wadogo Mchana (Day care) Dar es salaam(
UVIWADA )ikiwa ni mwendelezo wa Maadhimisho ya miaka 50 ya chuo cha
ustawi wa jamii.
Aidha
amesema kwamba Serikali kupitia Wizara hiyo haitawavumilia wamiliki wa Vituo
vya kulelea Watoto Mchana watakaobainika kwenda kinyume na Maadili na Desturi
za kitanzania.
Amesema
wamiliki wa Vituo vya Kulelea Watoto Mchana wanapaswa kutambua na kuzingatia
sheria, Kanuni na Miongozo mbalimbali iliyowekwa na Serikali katika uendelezaji
wa vituo hivyo.
"Mmiliki yeyote atakayebainika kwenda kinyume na maadili na desturi za
kitanzania nitafika nae mbali kisheria, hivyo nawasihi sana UVIWADA muungane
wenyewe, mshauriane wenyewe, mtiane moyo wenyewe ili muweze kuwabaini
wanaokwenda kinyume na maadili ya kitanzania"amesisitiza Dkt Gwajima
Aidha
ameupongeza UVIWADA kwa kazi kubwa ambayo wamekuwa wakiifanya katika jamii
kwani wamekuwa wakiwafanya watoto wa
Taifa hili kuwa na maadili mema pamoja na kuwakinga na vitendo vya ukatili.
Pia
Dkt Gwajima ambaye amekua mlezi wa UVIWADA ameahidi kuwa nao bega kwa bega katika
kuhakikisha malezi ya watoto yanatolewa kwa misingi bora nakuweza kuwa na
ustawi mzuri wa watoto.
katibu wa UVIWADA Josephine Rutashobya
Awali
katibu wa UVIWADA Mkoa wa Dar es salaam Josephine Rutashobya akiwasilisha risala
ya Umoja huo aliiomba Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya
Jamii,Jinsia na Makundi Maalumu kuangalia kwa mapana zaidi masharti ya usajili
wa vituo vyao kulingana na mazingira halisi hususani Jijini Dar es salaam.
Aidha
umoja huo pia uliiomba na kuishauri Serikali kutovifungia vituo ambavyo
bado havijapata usajili na badala yake viongezewe muda walau hadi mwezi
June 2024 ili viendelee na mchakato wa
usajili.
Pia wameiomba Serikali kuruhusu vituo hivyo
viruhusiwe kuwa na watoto hadi miaka sita,na mwongozo wake uboreshwe kwa madai
kuwa shule za awali ni chache,nakwamba shule za Serikali zisichukue watoto wa
chini ya miaka mitano maana huko hakuna uchangamfu wa awali wa watoto.
Maombi
mengine ni pamoja na vituo vya kulelea watoto Wadogo Mchana kua vinatoa huduma
tu kwenye jamii hivyo Serikali ivipunguzie mzigo wa Kodi.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa UVIWADA
Shukuru Mwakasege amesema kuwa asilimia kubwa ya Wamiliki wa
vituo vya kulelea watoto mchana hawajasajiliwa kutokana na sababu mbalimbali
ikiwemo masharti magumu nakuiomba serikali kupunguza masharti hayo.
Hata
hivyo Mwakasege amesema wataendelea kushirikiana na Serikali katika
kuhakikisha maelekezo yote yaliyotolewa wanayafanyia kazi.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni