Katibu wa Itikadi na Uenezi Paul Makonda amesema kwamba Maoni ya Wananchi juu ya Dira ya Maendeleo ya Taifa kwa Miaka thelathini ni muhimu hivyo amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika utoaji wa maoni kwa tume maalumu iliyoundwa kukusanya maoni hayo.
Hayo ameyasema Desemba 21,2023 jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari katika kutoa tathmini ya robo Mwaka ya CCM ambapo amesisitiza kuwa tayari sheria imeshapitishwa na bunge hivyo ni jukumu la kila Mwananchi kutoa maoni ya nini anataka kiwekwe katika dira hiyo
"Niwaombe wananchi
kujitokeza kwa wingi katika suala zima la utoaji wa maoni ya nini wanachotaka
kiwekwe kwenye dira ya Maendeleo ya Taifa , na Mpango huu utawafikia wananchi
wote kwa sababu tayari tume maalum imewekwa kwa ajili ya kukusanya maoni hayo',amesema
.
Sambamba na hayo katibu huyo Mwenezi wa CCM ameonyeshwa kukerwa
na na kitendo cha ukatikaji wa umeme
mara kwa mara na kuwataka viongozi wa Shirika la Ugavi wa Umeme Nchini
(TANESCO)kujitathimini bila kusubiri kuchukuliwa hatua.
Amesema hivi
karibuni Tanesco wamemuahidi Rais Samia ya kwamba ifikapi Januari kuwa kinu cha
umeme kitawashwa hivyo ni vyema ahadi hii ikatekelezwa kwa vitendo.
Aidha amewataka
watendaji wote kuanzia ngazi shina hadi mkoa kusikiliza kero za wananchi Ila
kutatua changamoto zinazowakabili.
" Nataka
niwakumbushe ndugu viongozi tuliopewa dhamana Na Rais Samia ya kuwatumikia
wananchi ni vyema tukatekeleze wajibu wetu tusisubiri mpaka Rais Samia anzishe
ziara aanze kasimamishwa njiani na wananchi ili watoe malalamiko
yao,"amesema Makonda.
Akizungumzia suala la
kuelekea uchaguzi wa serikali za Mitaa Makonda amesema ni vyema wanachama wenye
nia ya kugombea uongozi kuacha viongozi waliopo madarakani waendelee kutekeleza
majukumu yao kwa kuwa wao bado ni viongozi Halali wanaotambulika kisheria.
"Najua wapo watu
ambao wameanza kampeni za hapa Na pale Mimi niwambie tu ndugu zangu waacheni
viongozi wafanye kazi kwa sababu muda wao haujaisha Na wao bado ni viongozi
wanaotambulika na bado wanahaki ya kuwatumikia wananchi", amesema Makonda.
Hata hivyo Pauli
Makonda amebainisha kuwa kuanzia Januari 13 /2024 ataanza ziara ya kikazi
katika mikoa 10 ikiwemo
Tanga,Pwani,Kilimanjaro,Arusha,Manyara,Singinda,Tabora,Shinyanga na
Simiu.
Ambapo amewataka
watendaji wa halmashauri zote watakaopitiwa na ziara hiyo waanze kujitathmini
kabla ya kiongozi huyo kupita maeneo hayo.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni