Kamishna Jeneral wa DCEA Aretas Lyimo
Na Mussa Augustine.
Mamlaka ya Kudhibiti
na Kupambana na Dawa za Kulevya DCEA
imetoa onyo kwa wote wanaoendelea kujihusisha na biashara ya Dawa za kulevya
nchini Tanzania badala yake wajikite kwenye biashara nyingine halali kwani Mamlaka
hiyo imejidhatiti kukomesha biashara hiyo kwa kufanya oparesheni katika maeneo
mbalimbali nchini.
Onyo hilo limetolewa
Desemba 27,2023 Jijini Dar es salaam na Kamishna Jeneral wa DCEA Aretas Lyimo wakati
wa Mkutano wake na Waandishi wa habari kuelezea Mafanikio ya oparesheni maalumu
inayofanywa na Mamlaka hiyo katika kudhibiti biashara ya Dawa za Kulevya Nchini.
Kamishna Lyimo amesema
kwamba Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya Tanzania DCEA imekamata
jumla ya kilogram 3182 za dawa za kulevya aina ya Heroin na Methamphetamine
katika oparesheni maalum iliyofanyika jijini Dar es Salaam na Iringa kati ya
tarehe 5 hafi 23 mwezi Dicemba mwaka 2023.
Aidha ameendlea kusema
kuwa kuwa katika oparesheni hiyo jumala ya watu saba wamekamatwa kuhusika na
dawa hizo ambapo wawili kati yao wana asili ya Asia.
Amesema kuwa,kiasi
hiko cha dawa za kulevya ambacho hakijawai kukamatwa katika historia ya
Tanzania tangu kuanza kwa shughuli za udhibiti wa dawa za kulevya, hivyo
watuhumiwa waliokamatwa ni miongoni mwa mitandao mikubwa ya wauzaji wa dawa za
kulevya inayofuatiliwa nchini na duniani.
Aidha amesema kwamba Kiasi hicho cha
dawa za kulevya kinajumuisha kilogramu 2,180,29 za dawa aina ya methamphetamine
na kilogramu 1001.71 aina ya heroin zilizokamatwa katika wilaya za kigamboni, ubungo
na kinondoni jijini Dar es Salaam pamoja na Wilaya ya Iringa Mkoani
Inringa.
Aidha, dawa hizo
zilizokamatwa zilikuwa zimefungashwa kwenye vifungashio zenye chapa mbalimbali
za kahawa na majaninya chai ambapo mbinu hiyo inatumika kwa lengo
labusafirishaji wake na kukwepa kubainika.
Hata hivyo, amesema
kuwa dawa aina ya methamphetamine ni dawa mpya ya kulevya iliyopo katika kundi
la vichangamshi sawa cocaine ambapo dawa hiyo huwa kwenye mfumo wa vidonge,
unga au chembembe mithili ya chunvi ang'avu yenye rangi mbalimbali ambayo
huzalishwa kwenye maabara bubukwa kuchanganya aina mbalimbali za kemikali
bashirifu.
"Dawa hii ni
hatari kwa afya ya mtumiaji madhara yake ni makubwa na hayatibiki kirahisi
kwani mtumiaji hupata madhara ya kudumu kwenye ubongo na hivyo hupunguza uwezo
wa kutunza kumbukumbu kusababisha uraibu na kuathiri mfumo mzima wa faham;.Amesema Kamishna Lyimo
Kamishna huyo ameongeza
kuwa, kiasi cha dawa za kulevya zilizokamatwa zingefanikiwa kuingia Mtaani
zingeweza kuathiri zaid ya watu 76, 368,000 kwa siku hivyo, ukamataji huo
umeokoa nguvu kazi ambayo ingeangamia kutokana na madhara yatokanayo na madawa
ya kulevya ndani na nje ya nchi.
Katika hatua nyingine Kamishna Lyimo ameishukuru Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiwezesha Mamlaka hiyo katika kutekeleza
kazi zake kwa ufanisi mkubwa.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni