Zinazobamba

WANANCHI KATA YA TABATA WAILALAMIKIA KAMPUNI MPYA YA UZOAJI TAKA.

 

Taka ambazo zimelundikwa kwenye chumba maalumu kutokana na kushindwa kuzolewa kwa wakati katika Mtaa wa Tenge Kata ya Tabata.

Na Mussa Augustine.

Wananchi wa Kata ya Tabata Manispaa ya Ilala Mkoani Dar es salaam wameilalamikia Kampuni ya PB URASA LOGISTICS ambayo imepewa zabuni ya kuzoa taka  kwa kushindwa kuzoa taka kwenye mitaa yao tangu Kampuni hiyo ipewe kazi hiyo Novemba Mosi ,2023.

Malalamiko hayo wameyatoA Novemba 15,2023 kwa nyakati tofauti wakati wakizungumza na waandishi wa habari waliotembelea katani humo kujionea adha wanayoipata Wananchi hao ikiwemo harufu mbaya itokanayo na taka hizo hali ambayo pia inahatarisha afya zao kutokana na mripuko wa magonjwa ya kipindupindu.

“Tangu mwezi huu wa kumi na moja uanze sijawahi kuona gari la taka linapita kuzoa taka,nalipa hela ya taka kama kawaida lakini sipati huduma ,angalieni humu ndani taka zimejaa hadi funza wanatoka  hii ni hatari sana kwa afya yetu “amesema Bibi Lulu ambaye ni Mkazi wa Mtaa wa Tenge uliyopo katika kata ya Tabata.

Nae Linah Shayo mkazi wa Tabata Bima Mtaa wa Mengwe amebainisha kuwa hana taarifa kama kuna Mkandarasi mpya ambaye amepewa Zabuni hiyo nakwamba wananchi  wanapaswa kushirikishwa kutoa maoni yao pindi Mkandarasi mpya anapotafutwa ,lakini kwa Mkandarasi Mpya PB URASA LOGISTICS aliyepo kwa sasa Wananchi wanadai hawajashirikishwa na uongozi wa kata hiyo.

“Sisi tunatoa pesa zetu bila shida lakini Mkandarasi aliyeletwa kwa sasa hatoi taka kwa wakati,pia anabagua wenye pesa nyingi(matajiri) wanapata huduma kwa wakati lakini sisi Maskini ambao tunatoa pesa kidogo hatupewi huduma “amezungumza kwa uchungu Linah mbele ya Waandishi wa habari.

Nakuongeza “gari likipita taka zetu zinakua nje lakini zinaachwa hivyo inatubidi tena kuzirudisha ndani,hatuelewi ana maana gani huyu Mkandarasi mpya (PB URASA LOGISTICS) au anataka tutupe hizi taka barabarani ,tupeni ruhusa tutupe tumechoka”amesema Linah

Stanley Harold Mkazi wa Mtaa wa Umoja Road Mkandarasi aliyesitishiwa Mkataba wake (BUSAE COMPANY LTD )hakua na tatizo lolote katika utoaji huduma kwa Wananchi kwani alikua akifika kwa wakati kutoa taka hizo tofauti na aliyepo kwa sasa ambaye amesema inawezeka hana vitendea kazi vya kutosha.

“Inawezekana ni hila tu wamemfanyia mkandarasi wa zamani,lakini Mnyonge Mnyongeni  haki yake mpeni Mkandarasi wa Zamani(BUSAE COMPANY LTD )alikua na Vitendea kazi vya kutosha na alikua anatimiza wajibu wake ipasavyo,inawezekana kuna tofauti zao na viongozi wa kata yetu ,ndiyo maana wamemtoa lakini sisi wananchi tunaomba waondoe tofauti hizo wamrudishe mkandarasi wa zamani”amesema Stanley

Hata hivyo Afisa Mtendaji wa Kata ya Tabata aliyefahamika kwa jina moja la Mapesa hakua tayari kutoa ufafanuzi juu ya malalamiko hayo kwa madai kuwa mwenye mamlaka ya kuzungumzia sakata hilo ni Mkurugenzi wa Jiji la Dares salaam.


aka ambazo zimelundikwa kwenye chumba maalumu kutokana na kushindwa kuzolewa kwa wakati katika Mtaa wa Tenge Kata ya Tabata.

Kwa upande wake Meneja wa Kampuni ya Zamani iliyositishiwa Mkataba Oktoba 31,2023 ya BUSAE COMPANY LTD Faraja Adamu amebainisha kuwa walipata barua kutoka ofisi ya Mtendaji wa Kata hiyo ikiwataka kusitisha huduma ya kuzoa taka katani humo bila kuelezwa sababu zilizopelekea kufikiwa kwa maamuzi hayo.

“Hatujui sababu ni nini mpaka tunasitishiwa mkataba ,kama kulikwa na dosari tungeelezwa lakini tumeshangaa analetwa mkandarasi mpya ambaye tangu tarehe 1,mwezi huu wa 11 hajazoa taka na hali ni mbaya mtaani,Wananchi wanatupigia simu sisi kwani bado wanajua kuwa  tunatoa huduma”amesema Fraja.

Nakuongeza kuwa mwezi wa kumi tumeingiza magari mengi barabarani kuzoa taka,na kila mtaa ambao tumepita wenyeviti wa mtaa walikuawa wakisaini dispachi yetu,tumesitishiwa mkataba tukiwa tumeshazoa taka zote na mwezi huu wa kumi na moja tunaendelea na ukusanyaji wa madeni ya fedha za taka kutoka kwa wanachi  ambazo niza  huduma ya mwezi wa kumi.

Aidha Faraja ameongeza  kuwa wamepewa siku kumi na tisa pekee za kukusanya fedha hizo huku akidai kuwa kwa utaratibu  wanapaswa kupewa siku thelathini za kukusanya fedha hizo yaani kuanzia Novema 1 hadi Novemba thelathini mwaka huu,hivyo wameiomba ofisi ya Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaa kuingilia kati sakata hilo.

 

 

 

Hakuna maoni