CHIFU SANGALALI AWAHIMIZA WANANCHI KUJITOKEZA MATEMBEZI YA AMANI YA JMAT.
Na Mussa Augustine.
Mwenyekiti wa Machifu Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Nchini humo( JMAT) Chifu Antonia Sangalali
amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika Matembezi ya Amani
yatakayofanyika Desema 2 ,203 jijini Dar es salaam.
Rai hiyo ameitoa Novemba 21,2023 jijini Dar es salaam
wakati akizungumza na Waandishi habari ikiwa
ni mwendelezo wa kutoa taarifa ya maandalizi ya Matembezi hayo yenye lengo la
kuiunga Mkono Serikali ya Dkt.Samia Suluhu Hasssan katika kudumisha Amani
Nchini.
“Mimi ni chifu wa kabila la Wasukuma Mkoani Simiyu
lakini pia ni Mwenyekiti wa Machifu Tanzania,pia ni Mjumbe wa JMAT ,hivyo
katika matembezi hayo kutakuwepo na tisheti maalumu ambazo tutazivaa kwa yeyote
anayehitaji zinapatika hapa ofisi za JMAT na utaratibu wa kuzipata utatangazwa
na uongozi “amesema Chifu Antonia.
Nakuongeza kuwa”naomba wanachi wajitokeze kwa wingi
katika matembezi hayo ili tumuunge mkono Rais Wetu Mpendwa Dkt Samia Suluhu
Hassan katika kuhimiza kwa vitendo kudumisha amani katika Taifa letu,kwani
amani inatokana na sisi wenyewe.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni