Zinazobamba

UONGOZI MPYA TCCIA UMEAHIDI MAGEUZI MAKUBWA YA MAENDELEO SEKTA BINAFSI

 

Na Mussa Augustine

Rais Mpya wa Chemba ya Biashara,Viwanda na Kilimo Tanzania(TCCIA) Vicent Bruno Minja amesema kuwa uongozi wake unatarajia kufanya mambo makubwa ndani ya siku miamoja ikiemo kuimarisha Ushirikiano wa dhati kati ya Wanachama ,Wafanyabiashara na Wadau wote ili kuhakikisha sauti za wanachama zinasikika na kuzingatiwa katika kila hatua inayochukuliwa.

Hayo ameyasema Novemba 10,2023 Jijini Dar es salaam  wakati akizungmza na waandishi wa habari kwa lengo la kutangaza rasmi bodi mpya ya TCCIA iliyochaguliwa hivi karibuni kupitia Mkutano Mkuu Maalumu uliyofanyika  Novemba 7 ,2023 jijini humo.

Aidha Rais Minja amesema kuwa Mwelekeo na Mpango Mkakati wa uongozi huo ni pamoja na Kukuza Maendeleo ya Sekta za Biashara,Viwanda na Kilimo kwa kushirikiana na Serikali na Wadau wengine kwa kuweka mikakati imara ya kuvutia uwekezaji,kutoa mafunzo na kusaidia miradi inayochangia ukuaji wa sekta hizo muhimu.

Rais huyo wa TCCIA amendelea kutaja mikakati mingine kuwa ni pamoja na Kuendeleza Ubunifu na teknolojia katika utoaji wa Vyeti Vya uasili,Kukuza Umoja na Mshikamano ndani ya Chemba ,Kuimarisha ushirikiano na Serikali ,Taasisi ,Balozi na Wadau wa Maendeleo ,Kusimamia Mabaraza ya Biashara na Kuendelea kuhudumia Sekta Bianafsi Nchini.

''Tutatumia uzoefu wetu wa miaka 35 katika huduma na uongozi wa sekta Binafsi nchini kusimamia Mabaraza ya Biashara na kuendelea kutoa huduma bora kwa sekta binafsi'',amesisitiza Rais Minja.

Kwa Upande wake Makamu mpya wa rais Sekta ya Kilimo Swallah Swallah amesema kuwa Sekta ya Kilimo ni Muhimili Muhimu wa TCCIA,nakwamba  asilimia karibia kubwa ya Wananchi wapo katka sekta ya kilimo hivyo Chemba hiyo itashirikiana na serikali kuhakikisha wakulima wanapata pembejeo za kilimo kwa wakati lakini pia kupata  masoko ya uhakika.

 Aidha Swallah ameongeza kuwa  ‘’TCCIA kupitia sekta ya Kilimo tutahakikisha mazao yanayozalishawa na Wakulima yanapata soko la uhakika,pia kushirikiana na serikali kupitia program yake ya kuendeleza sekta ya Kilimo nchini,ili kuongeza uzalishaji wa Mazao nakua na kilimo chenye tija kwa Wakulima na Taifa kwa ujumla’’.

 Nae Makamu Rais Biashara TCCIA, Boniphace Ndengo amebainisha kuwa atahakikisha anachochea Mageuzi ya Masoko ya ndani na kimataifa ,kuwezesha kupata Mitaji ya kukuza  biashara ili kuifanya Sekta Binafsi kukua na kuchangia kwa kiasi kikubwa Maendeleo ya Taifa.

 ‘’Tutahakikisha tunatumia fursa zilizopo kuanzisha mfuko Maalumu wa kutoa mikopo ya mitaji ya biashara,kuimarisha biashara pamoja na kujenga makampuni makubwa ya Biasha hapa nchini’’amesema Ndengo.

 Mkutano Mkuu Maalumu ulioketi Novemba 7,2023 jijini Dar es salaam ,ulihudhuriwa na Wajumbe kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara,ulifanya uchaguzi wa viongozi mbalimbali wa kitaifa ambapo Vicent Minja alichaguliwa kishika nafasi ya Rais wa Chemba hiyo,huku Boniphace Ndengo akiwa Makamu Rais Biashara,na Swallah Swallah akiwa Makamu Rais Kilimo wa TCCIA.

Hakuna maoni