Zinazobamba

DKT ALHAD MUSSA AWASIHI WANANDOA KUISHI KWA UAMINIFU




Na Mussa Augustine.

Mwenyekiti Taifa wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Sheikh Dkt, Alhad Mussa Salum amesema ilikuondoa suala la kutoaminiana kwa wanandoa hawanabudi kuachana na taarifa za kinafiki baina yao kutoka kwa wafitini.

Hayo yamesemwa Oktoba 31,2023 na Sheikh Dkt.Alhad Mussa alipozungumza na Waandishi wa habari ofisini kwakwe Jijini Dar es salaam,kufuatia kuwepo kwa tatizo  kubwa la wanandoa kwenda katika vituo vya afya kupima DNA za watoto kwakile kinachoitwa kukosekana kwa uaminifu baina ya wanandoa.

“Kwanza watanzania hawanabudi kutambua kwamba ninayoyasema ni kwa niaba ya JMAT na si vinginevyo wakati uliopita nilikuwa nina kofia mbili hii ya JMAT na ya Sheikh Mkoa wa Dar es Salaam, lakini sasa nazungumza kwa niaba ya Taasisi kubwa,tatizo lipo, kikubwa nikuwa na hofu ya Mungu,tukiwa na hofu ya Mwenyezi Mungu tutakuwa salama pasipo hivyo kuiona pepo itakuwa aghalabu” amesema Sheikh Dkt .Alhad Mussa

Amesema dhambi ifanywayo na binadamu wa karne hii ni kufulu zaidi ya ile ya Sodoma na gomora, kwakuwa imefikia mahala sasa wanaume kwa wanaume wanahitaji kufunga ndoa kwa kile wanachokiita haki za binadamu ni upuuzi na ujinga kwa binadamu waliostaarabika ,sodoma walifanya kwa siri sasa ni bayana jambo ambalo halikubaliki mbele za Mungu.

Aidha Sheikh Dkt Mussa amesema ili kuepuka dhambi itokanayo na zinaa,wanandoa wote wawili wa kiume na kike hawanabudi kuachana na tabia mbaya ya kutoka nje ya ndoa,kwani dhambi hiyo ni kubwa kuliko wanandoa wanavyofikiria kwao ni dogo, lakini wanayemkosea halioni dogo na adhabu yake siku ya kiama ni kubwa.

Vilevile amesema yapo makosa yanayofanywa na wanaume kwa hoja ambazo hazina mashiko hata kidogo, kumbagugua au kumkataa mtoto kwa kigezo cha rangi na maumbile, hadi kufikia kupima DNA bahati nzuri awe wake asipo kuwa wake atakuwa ameathirika kisaikolojia kwa kiasi kikubwa.

Sheikh Dkt Mussa ameongeza kuwa kadhia kubwa katika wimbi hili kubwa la watu kupima DNA ni kutoaminiana baina ya wanadamu huku akiwaomba watanzania kuzingatia tamaduni za nje na kitanzania ambazo ni nzuri.



Hakuna maoni