Zinazobamba

S3 EDUCATION YATOA FURSA KWA WANAFUNZI WA KITANZANIA KUTAFUTA VYUO VIKUU NJE YA NCHI.


Na Mussa Augustine.

Katika kuunga Mkono jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kukuza sekta ya Elimu, taasisi inayojihusisha na Masuala ya  Maonyesho ya Elimu ya Vyuo vikuu  S3 Education imefanya maonesho hayo  kwa kukutanisha vyuo vikuu  mbalimbali kutoka nje ya Nchi.

Akizungumza Oktoba 10 ,2023  Katika Maonesho hayo yaliyofanyika katika hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam,Meneja wa Taasisi hiyo, Fatema Salemwalla, amesema kuwa Maonesho hayo yatawasadia wanafunzi kupata uelewa mpana wa kozi ambazo wanahitaji kwenda kuzisoma nje ya nchi kwa kukutanisha moja kwa moja na wahusika wa vyuo hivyo.

Aidha Fatema  amesema kuwa Kwenye Maonesho hayo zaidi ya wanafunzi 500 kutoka shule mbalimbali wametembelea  katika mabanda ya vyuo hivo nakuweza kujionea fursa mbalimbali za kielimu kutoka katika vyuo vikuu vya Nje ya Nchi ya Tanzania  ikiwemo Vyuo Vikuu vya nchini Mauritius,UK,Canada,USA,pamoja Ujerumani.

"Maonesho haya huwa tunayafanya mara mbili kwa mwaka,lengo ni kutoa fursa kwa vyuo hivi vikuu nje ya nchi kutangaza kozi zao,tunawaalika wanafunzi kupitia shule zao kuja kutembelea maonesho haya,na sasa hivi teknolojia imekuwa kubwa,wanafunzi wanafanya utafiti mapema wa kujua kozi ambazo wanahitaji kusoma kabla hata hawajafika kwenye vyuo husika"amesema Fatema na kuongeza kuwa,

"Tupo hapa na idadi ya vyuo vikuu 12 kutoka nje ya nchi ambavyo vimeshiriki Katika maonesho haya na tunahitaji tuendelee kutafuta vyuo vingine zaidi ili kutoa fursa kubwa zaidi kwa wanafunzi wa Kitanzania kutimiza ndoto zao za kielimu kwenda kusoma nje ya nchi"

 Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi waliotembelea maonesho hayo akiwemo  Mwanafunzi Maryam Suleiman anayesoma kidato cha sita katika shule ya Shaaban Robert iliyopo Jijini Dar es salaam ameipongeza taasisi hiyo nakusema kwamba maonesho hayo yatawasadia kama wanafunzi wa Tanzania kutimiza ndoto zao za kusoma nje ya nchi.

"Leo tumepata fursa kubwa ya kutambua vyuo vikuu mbalimbali nje ya nchi ambavyo vina kozi tunazozipenda na wazazi wetu wanao uwezo wa kuvilipia ambavyo vitatupa elimu ambayo itatupa mwanga wa kuja kuwekeza hapa nchini Tanzania"amesema Maryam

 


Hakuna maoni