Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani).
Na Mussa Augustine.
Jeshi la Polisi Kanda
Maalum ya Dar es salaam limewatahadharisha
baadhi ya mashabiki wenye tabia ya kuwasha fataki au baruti
uwanjani,nakwamba atakayefanya hivo kisheria kali zitachukuliwa
dhidi yao.
Akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum
ya Dar es Salaam, SACP Jummane Muliro amesema kuwa Jeshi hilo linatambua
kuwa Ijumaa, Oktoba 20, 2023 kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam
kutakuwa na uzinduzi Mashindano ya“African football league”
ambapo pia kutakuwa na
mchezo wa soka hatua ya robo fainali ya mashindano hayo baina ya klabu ya
Simba ya Tanzania na Al Ahly ya nchini Misri utakaochezwa kuanzia majira
ya saa 12:00 jioni,ambapo mifumo ya Usalama imeimarishwa.
SACP Muliro amesema
kuwa, jeshi la Polisi linatambua mchezo huo utahusisha wageni kutoka nje
ya nchi na kuwa na mkusanyiko mkubwa katika kiwanja hicho, kutokana na
hali hiyo baadhi ya barabara zitafungwa ili kupunguza msongamano wa
kuelekea uwanjani hapo, hivyo mashabiki wa soka wafike mapema ili
kuepusba usumbufu unaoweza kuepukika.
"Jeshi la Polisi
limechukua tahadhari zote za kiusalama kabla, wakati na baada ya
mchezo huo, ukaguzi wa hali ya juu katika mageti ya kuingia na hairuhisiwa
mtu yeyote kwenda uwanjani na silaha ya aina yoyote, isipokuwa baadhi ya
vyombo vya dola vyenye jukumu la usalama eneo
hilo"amesema
Ameongeza kuwa,mtu
yoyote asiyekuwa na tiketi hataruhusiwa kusogelea uwanja huo au maeneo ya
milango ya kuingia ili usalama uimarishwe zaidi kutokana na uhalisia
wa kuwepo kwa watu wengi uwanjani hapo.
SACP Muliro ameongeza
kuwa jeshi la polisi halitavumilia tabia hizo na zingine ambazo zimepigwa
marufuku na vyama vya soka FIFA, CAF na TFFtabia ambazo zinaweza kupelekea
Tanzania kukosa sifa yakuandaa mashindano kama haya wakati mwingine.
"Watakao kaidi,
watakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria,Jeshi la Polisi linawatakia
mashabiki wa soka kushangilia kistaarabu nakuacha alama nzuri ya kiusalama
Katika Taifa la Tanzania" amesisitiza kwenye Mkutano huo na Waandishi wa
habari.
Katika hatua nyingine Kamanda huyo wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam SACP Muliro amewataka Mashabiki wanaoingia na watoto Uwanjani kuacha kuingia na watoto ambao hawana tiketi kwana wanakua hawana sehemu ya kukaa hivyo kusababisha usumbufu kwa Watu na usalama wao kwa ujumla.
Pia amesisitiza kuwa kuanzia sasa mifumo ya kupokea wageni wa Kimataifa imeimarishwa kutokea kwenye Uwanja Wa ndege hadi sehemu wanayofikia.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni